< Ayubu 5 >
1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
Ded zazivlji! Zar će ti se tko odazvat'? Kojem li se svecu misliš sad obratit'?
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
Doista, budalu njegov bijes ubija, luđaka će sasvim skončat ljubomora.
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
Bezumnika vidjeh kako korijen pušta, al' prokletstvo skoro na kuću mu pade.
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
Njegovi su sinci daleko od spasa, njih nezaštićene na Vratima tlače.
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
Ljetinu njihovu pojedoše gladni, sam Bog ju je njima oteo iz usta, a žedni hlepe za njihovim dobrima.
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
Ne, opačina ne izbija iz zemlje, nit' nevolja iz tla može nići sama,
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
nego čovjek rađa muku i nevolju kao što let orlov teži u visinu.
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
Al' ja bih se ipak Bogu utekao i pred njime stvar bih svoju razložio.
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
Nedokučiva on djela silna stvori, čudesa koja se izbrojit' ne mogu.
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
On kišom rosi po svem licu zemljinu i vodu šalje da nam polja natapa.
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Da bi ponižene visoko digao, da bi ojađene srećom obdario,
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
redom ruši ono što lukavci smisle, što god započeli, on im izjalovi.
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
On hvata mudre u njihovu lukavstvu, naume spletkara obraća u ništa.
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
Posred bijela dana zapadnu u tamu, pipaju u podne kao usred noći.
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
On iz njinih ralja izbavlja jadnika, iz silničkih ruku diže siromaha.
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
Tako se pokaže nada nevoljniku, i nepravda mora zatvoriti usta.
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
Da, blago čovjeku koga Bog odbaci! Stoga ti ne prezri karanje Svesilnog!
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
On ranjava, ali i ranu povija, udara i svojom zacjeljuje rukom.
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
Iz šest će nevolja tebe izbaviti, ni u sedmoj zlo te dotaknuti neće.
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
U gladi, od smrti on će te spasiti, a u ratu, oštru će te otet maču.
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
Biču zla jezika uklonit će tebe, ispred otimača bez straha ćeš biti.
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
Suši i studeni ti ćeš se smijati i od divljih zvijeri strahovati nećeš.
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
Sklopit' ti ćeš savez s kamenjem na njivi, zvjerad divlja s tobom u miru će biti.
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
U šatoru svome mir ćeš uživati, dom svoj kad pohodiš netaknut će stajat.
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
Koljeno ćeš svoje gledat' gdje se množi i potomstvo gdje ti kao trava raste.
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
U grob ti ćeš leći kada budeš zreo, kao što se žito snosi kad dozori.
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
Sve motrismo ovo: istina je živa! zato sve za dobro svoje ti poslušaj.”