< Ayubu 5 >

1 “Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
任你呼求,看有誰答應你﹖諸聖者中,看你轉向那一位﹖
2 Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
的確,憂憤殺死愚人,怒火使痴者喪生。
3 Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
我知道:愚人一根深蒂固,他的居所即被詛咒;
4 Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
他的子女,無人支援,在城門前被踐踏,無人救護。
5 Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
他們收穫的,飢餓者來吃;且將剩餘的,搶去儲存;他們的財富,為口渴者喝盡。
6 Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
因為災禍不是由土中而來,憂患不是生自地中;
7 Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
而是人自尋苦惱,如雛鷹自會飛翔。
8 “Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
如果是我,我必投奔天主,向天主陳訴我的案情。
9 Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
他所作的大事,高深莫測;他所行的奇事,不可勝數:
10 Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
他使雨落在地上,引水滋潤郊田;
11 Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
使卑微的人高昇,使受苦的人獲得救助;
12 Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
粉碎狡猾人的計謀,使他們的作為一無所成;
13 Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
以智者的計謀捕捉智者,使奸猾人的策畫即時成空;
14 Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
他們白日遇到黑暗,正午摸索如在夜間;
15 Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
他搭救被剝削者脫離人口,挽救窮人擺脫強暴的手。
16 Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
如此,貧苦的人獲得希望,邪惡將閉口無言。
17 “Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
的確,天主所懲戒的人是有福的:全能者的訓戒,你不可忽視。
18 Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
因為他打傷了,而又包紮傷口;他擊碎了,而又親手治療。
19 Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
你六次遭難,他次次拯救;到第七次,災難不會臨於你。
20 Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
饑饉中,他必救你不死;戰爭中,必使你得免刀劍。
21 Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
唇槍舌劍,你必能躲藏;大難來臨,你不必張惶;
22 Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
對大難和饑荒,你可置之一笑;對地上的野獸,也不用驚惶。
23 Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
你將與田野的頑石立約,曠野的猛獸必與你和好。
24 Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
你將見到你的帳幕平安無恙,察看羊欄時,一無所失。
25 Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
你將確知子孫繁昌,你的苗裔猶如田野青草。
26 Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
你必高年纔葬於墓,好像麥梱準時收藏。
27 “Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”
看,這是我們所觀察的真理,你若細聽,自會獲益良多。

< Ayubu 5 >