< Ayubu 42 >

1 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
Then Job, responding to the Lord, said:
2 “Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote, wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.
I know that you are able to do all things, and that no thoughts are hidden from you.
3 Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’ Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi, mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.
So, who is it that would disguise a lack of knowledge as counsel? Therefore, I have been speaking foolishly, about things whose measure exceeds my knowledge.
4 “Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena; nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’
Listen, and I will speak. I will question you, and you may answer me.
5 Masikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako, lakini sasa macho yangu yamekuona.
By paying attention with the ear, I have heard you, but now my eye sees you.
6 Kwa hiyo najidharau mwenyewe, na kutubu katika mavumbi na majivu.”
Therefore, I find myself reprehensible, and I will do penance in embers and ashes.
7 Baada ya Bwana kusema mambo haya yote na Ayubu, akamwambia Elifazi Mtemani, “Nina hasira juu yako na juu ya rafiki zako wawili, kwa sababu hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.
But after the Lord had finished speaking these words to Job, he said to Eliphaz the Themanite: My wrath has been kindled against you, and against your two friends, because you have not been speaking correctly in my eyes, as my servant Job has done.
8 Basi sasa chukueni mafahali saba na kondoo dume saba mkamwendee mtumishi wangu Ayubu nanyi mkatoe sadaka za kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe. Mtumishi wangu Ayubu ataomba kwa ajili yenu, nami nitayakubali maombi yake ili nisiwatendee sawasawa na upumbavu wenu. Ninyi hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.”
Therefore, have seven bulls and seven rams brought to you, and go to my servant Job, and offer these as a holocaust for yourselves. But also, my servant Job will pray for you; I will accept his face, so that foolishness will not be imputed to you. For you have not been speaking correctly about me, as my servant Job has done.
9 Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi wakafanya kama Bwana alivyowaambia; naye Bwana akayakubali maombi ya Ayubu.
So Eliphaz the Themanite, and Baldad the Suhite, and Zophar the Naamathite departed, and they did just as the Lord had spoken to them, and the Lord accepted the face of Job.
10 Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake, Bwana akamwondoa kwenye uteka, akamfanikisha tena naye akampa mara mbili ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzoni.
Likewise, the Lord was moved by the repentance of Job, when he prayed for his friends. And the Lord gave to Job twice as much as he had before.
11 Ndipo ndugu zake wote waume kwa wake na kila mtu aliyemfahamu mwanzoni, wakaja wakala pamoja naye katika nyumba yake. Wakamfariji na kumtuliza moyo juu ya taabu yote Bwana aliyoileta juu yake, nao kila mmoja akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu.
Yet all his brethren came to him, and all his sisters, and everyone who had known him before, and they ate bread with him in his house. They also shook their heads over him and comforted him, because of all the bad things that God had inflicted on him. And each one of them gave him one female sheep, and one earring of gold.
12 Bwana akaibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ile ya kwanza. Alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, ngamia elfu sita, jozi za mafahali elfu moja, na punda wa kike elfu moja.
And the Lord blessed the latter end of Job even more than his beginning. And he had fourteen thousand sheep, and six thousand camels, and a thousand pairs of oxen, and a thousand she-donkeys.
13 Tena alikuwa na wana saba na binti watatu.
And he had seven sons and three daughters.
14 Binti wa kwanza aliitwa Yemima, wa pili Kesia na wa tatu Keren-Hapuki.
And he called the name of one, Daylight, and the name of the second, Cinnamon, and the name of the third, Horn of Cosmetics.
15 Hapakuwepo mahali popote katika nchi ile yote palipopatikana wanawake wazuri kama binti za Ayubu; naye baba yao akawapa urithi pamoja na ndugu zao.
And, in the whole world, there were not found women so beautiful as the daughters of Job. And so their father gave them an inheritance along with their brothers.
16 Baada ya hili Ayubu akaishi miaka 140; akawaona wanawe na wana wa wanawe hata kizazi cha nne.
But Job lived long after these events, for a hundred and forty years, and he saw his children, and his children’s children, all the way to the fourth generation,
17 Hivyo Ayubu akafa, akiwa mzee aliyekuwa ameshiba siku.
and he died an old man and full of days.

< Ayubu 42 >