< Ayubu 42 >

1 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
Saa svarede Job HERREN og sagde:
2 “Ninajua ya kuwa unaweza kufanya mambo yote, wala hakuna mpango wako unaoweza kuzuilika.
Jeg ved, at du magter alt, for dig er intet umuligt!
3 Uliuliza, ‘Ni nani huyu afichaye mashauri yangu bila maarifa?’ Hakika nilisema juu ya mambo niliyokuwa siyaelewi, mambo ya ajabu mno kwangu mimi kuyajua.
»Hvem fordunkler mit Raad med Ord, som er uden Indsigt?« Derfor: jeg talte uden Forstand om noget, som var mig for underfuldt, og som jeg ej kendte til.
4 “Ulisema, ‘Sikiliza sasa, nami nitanena; nitakuuliza swali, nawe yakupasa kunijibu.’
Hør dog, og jeg vil tale, jeg vil spørge, og du skal lære mig!
5 Masikio yangu yalikuwa yamesikia habari zako, lakini sasa macho yangu yamekuona.
Jeg havde kun hørt et Rygte om dig, men nu har mit Øje set dig;
6 Kwa hiyo najidharau mwenyewe, na kutubu katika mavumbi na majivu.”
jeg tager det derfor tilbage og angrer i Støv og Aske!
7 Baada ya Bwana kusema mambo haya yote na Ayubu, akamwambia Elifazi Mtemani, “Nina hasira juu yako na juu ya rafiki zako wawili, kwa sababu hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.
Men efter at HERREN havde talet disse Ord til Job, sagde han til Temaniten Elifaz: »Min Vrede er blusset op mod dig og dine to Venner, fordi I ikke talte rettelig om mig som min Tjener Job!
8 Basi sasa chukueni mafahali saba na kondoo dume saba mkamwendee mtumishi wangu Ayubu nanyi mkatoe sadaka za kuteketezwa kwa ajili yenu wenyewe. Mtumishi wangu Ayubu ataomba kwa ajili yenu, nami nitayakubali maombi yake ili nisiwatendee sawasawa na upumbavu wenu. Ninyi hamkusema yaliyo sawa kwa habari yangu, kama alivyosema mtumishi wangu Ayubu.”
Tag eder derfor syv Tyre og syv Vædre og gaa til min Tjener Job og bring et Brændoffer for eder. Og min Tjener Job skal gaa i Forbøn for eder, thi ham vil jeg bønhøre, saa jeg ikke gør en Ulykke paa eder, fordi I ikke talte rettelig om mig som min Tjener Job!«
9 Kwa hiyo Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi wakafanya kama Bwana alivyowaambia; naye Bwana akayakubali maombi ya Ayubu.
Saa gik Temaniten Elifaz, Sjuhiten Bildad og Na'amatiten Zofar hen og gjorde, som HERREN havde sagt, og HERREN bønhørte Job.
10 Baada ya Ayubu kuwaombea rafiki zake, Bwana akamwondoa kwenye uteka, akamfanikisha tena naye akampa mara mbili ya vile alivyokuwa navyo hapo mwanzoni.
Og HERREN vendte Jobs Skæbne, da han gik i Forbøn for sine Venner; og HERREN gav Job alt, hvad han havde ejet, tvefold igen.
11 Ndipo ndugu zake wote waume kwa wake na kila mtu aliyemfahamu mwanzoni, wakaja wakala pamoja naye katika nyumba yake. Wakamfariji na kumtuliza moyo juu ya taabu yote Bwana aliyoileta juu yake, nao kila mmoja akampa kipande cha fedha na pete ya dhahabu.
Saa kom alle hans Brødre og Søstre og alle, der kendte ham tilforn, og holdt Maaltid med ham i hans Hus, og de viste ham deres Medfølelse og trøstede ham over al den Ulykke, HERREN havde bragt over ham, og de gav ham hver en Kesita og en Guldring.
12 Bwana akaibariki sehemu ya mwisho ya maisha ya Ayubu kuliko ile ya kwanza. Alikuwa na kondoo elfu kumi na nne, ngamia elfu sita, jozi za mafahali elfu moja, na punda wa kike elfu moja.
Og HERREN velsignede Jobs sidste Tid mere end hans første. Han fik 14 000 Stykker Smaakvæg, og 1000 Aseninder.
13 Tena alikuwa na wana saba na binti watatu.
Og han fik syv Sønner og tre Døtre,
14 Binti wa kwanza aliitwa Yemima, wa pili Kesia na wa tatu Keren-Hapuki.
og han kaldte den ene Jemima, den anden Kezia og den tredje Keren-Happuk.
15 Hapakuwepo mahali popote katika nchi ile yote palipopatikana wanawake wazuri kama binti za Ayubu; naye baba yao akawapa urithi pamoja na ndugu zao.
Saa smukke Kvinder som Jobs Døtre fandtes ingensteds paa Jorden; og deres Fader gav dem Arv imellem deres Brødre:
16 Baada ya hili Ayubu akaishi miaka 140; akawaona wanawe na wana wa wanawe hata kizazi cha nne.
Siden levede Job 140 Aar og saa sine Børn og Børnebørn, fire Slægtled.
17 Hivyo Ayubu akafa, akiwa mzee aliyekuwa ameshiba siku.
Saa døde Job gammel og mæt af Dage.

< Ayubu 42 >