< Ayubu 40 >

1 Bwana akamwambia Ayubu:
Dios siguió hablando a Job.
2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
“¿Todavía vas a pelear con el Todopoderoso y tratar de enderezarlo? Quien discute con Dios debe dar alguna respuesta”.
3 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
Job respondió al Señor:
4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
“Yo no soy nada. No tengo respuestas. Pongo mi mano delante de mi boca.
5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
Ya he dicho demasiado y no diré nada más”.
6 Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
Entonces el Señor respondió a Job desde el torbellino:
7 “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
“Prepárate, sé fuerte, porque voy a interrogarte y debes responderme.
8 “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
“¿De verdad vas a decir que mis decisiones están equivocadas? ¿Vas a condenarme para tener razón?
9 Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
¿Eres tan poderoso como yo? ¿Truena tu voz como la mía?
10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
¿Por qué no te vistes de majestad y dignidad, y te revistes de gloria y esplendor?
11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
Da rienda suelta a tu feroz ira. Humilla a los soberbios con una mirada.
12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
Derriba a los soberbios con tu mirada; pisotea a los malvados allí donde están.
13 Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
Entiérralos en el polvo; enciérralos en la tumba.
14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
Entonces también estaré de acuerdo en que tu propia fuerza puede salvarte.
15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
“Considera a Behemot, una criatura que hice igual que a ti. Come hierba como el ganado.
16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
Mira sus poderosos lomos, los músculos de su vientre.
17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
Dobla su cola como un cedro; los tendones de sus muslos son fuertes.
18 Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
Sus huesos son como tubos de bronce, sus miembros como barras de hierro.
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
Es el ejemplo más importante de lo que Dios puede hacer; sólo el que lo hizo puede acercarse a él con una espada.
20 Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
Las colinas producen alimento para él, y todos los animales salvajes juegan allí.
21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
Se encuentra bajo el loto; se esconde en los juncos del pantano.
22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
El loto la cubre de sombra; los sauces del valle la rodean.
23 Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
Aunque el río se desborde, no se preocupa; permanece en calma cuando el río Jordán se agita contra él.
24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?
Nadie puede atraparlo mientras mira, ni perforar su nariz con un lazo”.

< Ayubu 40 >