< Ayubu 40 >

1 Bwana akamwambia Ayubu:
Se dirigió entonces Yahvé a Job y dijo:
2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
“Quiere el censor contender más con el Omnipotente? El que disputa con Dios responda.”
3 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
Job respondió a Yahvé y dijo:
4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
“He aquí ¡cuán pequeño soy yo! ¿Qué puedo responderte? Pondré mi mano sobre mi boca.
5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
Una vez he hablado, mas no hablaré más; y otra vez (he hablado), pero no añadiré palabra.
6 Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
Yahvé siguió hablando a Job desde el torbellino, y dijo:
7 “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
“Cíñete los lomos como varón; voy a preguntarte y tú me instruirás.
8 “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
¿Quieres tú de veras negar mi justicia, condenarme a Mí para justificarte a ti mismo?
9 Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
¿Tienes tú un brazo como el de Dios, y puedes tronar con voz semejante a la suya?
10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
Adórnate de alteza y majestad, y revístete de gloria y grandeza.
11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
Derrama los torrentes de tu ira; mira a todo orgulloso y humíllalo.
12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
Mira a todo soberbio y abátelo, aplasta a los malvados donde estén.
13 Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
Escóndelos a todos en el polvo, y cubre su rostro con tinieblas.
14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
Yo entonces te alabaré, porque tu diestra podrá salvarte.
15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
Mira a Behemot, creado por Mí lo mismo que tú. Come hierba como el buey;
16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
y ve que su fuerza está en sus lomos, y su vigor en los músculos de su vientre.
17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
Endurece su cola como un cedro; y los nervios de sus muslos son como un solo tejido.
18 Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
Sus huesos son tubos de bronce, sus costillas como planchas de hierro.
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
Es la primera de las obras de Dios; Él que lo hizo le dio una espada.
20 Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
Los montes le ofrecen alimento, (alrededor de él) retozan todas las bestias del campo.
21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
Duerme debajo de los lotes, en la espesura de los juncos y pantanos.
22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
Los lotos le cubren con su sombra, y le rodean los sauces del río.
23 Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
Al desbordar el río no se amedrenta; se queda tranquilo aunque el Jordán le llegue a la garganta.
24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?
Fascina la (presa) con los ojos, y su nariz perfora las redes.

< Ayubu 40 >