< Ayubu 40 >
1 Bwana akamwambia Ayubu:
L’Eterno continuò a rispondere a Giobbe e disse:
2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
“Il censore dell’Onnipotente vuole ancora contendere con lui? Colui che censura Iddio ha egli una risposta a tutto questo?”
3 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
Allora Giobbe rispose all’Eterno e disse:
4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
“Ecco, io son troppo meschino; che ti risponderei? Io mi metto la mano sulla bocca.
5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
Ho parlato una volta, ma non riprenderò la parola, due volte… ma non lo farò più”.
6 Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
L’Eterno allora rispose a Giobbe dal seno della tempesta, e disse:
7 “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
“Orsù, cingiti i lombi come un prode; ti farò delle domande e tu insegnami!
8 “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
Vuoi tu proprio annullare il mio giudizio? condannar me per giustificar te stesso?
9 Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
Hai tu un braccio pari a quello di Dio? o una voce che tuoni come la sua?
10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
Su via, adornati di maestà, di grandezza, rivestiti di splendore, di magnificenza!
11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
Da’ libero corso ai furori dell’ira tua; mira tutti i superbi e abbassali!
12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
Mira tutti i superbi e umiliali! e schiaccia gli empi dovunque stanno!
13 Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
Seppelliscili tutti assieme nella polvere, copri di bende la lor faccia nel buio della tomba!
14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
Allora, anch’io ti loderò, perché la tua destra t’avrà dato la vittoria.
15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
Guarda l’ippopotamo che ho fatto al par di te; esso mangia l’erba come il bove.
16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
Ecco la sua forza è nei suoi lombi, e il vigor suo nei muscoli del ventre.
17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
Stende rigida come un cedro la coda; i nervi delle sue cosce sono intrecciati insieme.
18 Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
Le sue ossa sono tubi di rame; le sue membra, sbarre di ferro.
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
Esso è il capolavoro di Dio; colui che lo fece l’ha fornito di falce,
20 Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
perché i monti gli producon la pastura; e là tutte le bestie de’ campi gli scherzano intorno.
21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
Si giace sotto i loti, nel folto de’ canneti, in mezzo alle paludi.
22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
I loti lo copron dell’ombra loro, i salci del torrente lo circondano.
23 Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
Straripi pure il fiume, ei non trema; rimane calmo, anche se avesse un Giordano alla gola.
24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?
Potrebbe alcuno impadronirsene assalendolo di fronte? o prenderlo colle reti per forargli il naso?