< Ayubu 40 >

1 Bwana akamwambia Ayubu:
Et le Seigneur continua à parler à Job:
2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
Est-ce que celui qui dispute avec Dieu se réduit si facilement au silence? Certainement celui qui reprend Dieu doit lui répondre.
3 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
Répondant alors au Seigneur, Job dit:
4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
Moi qui a parlé légèrement, que peux-je répondre? Je mettrai ma main sur ma bouche.
5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
J’ai dit une chose (plut à Dieu que je ne l’eusse pas dite!) et une autre; je n’y ajouterai rien de plus.
6 Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
Or, répondant à Job du milieu d’un tourbillon, le Seigneur dit:
7 “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
Ceins tes reins comme un homme de cœur; je t’interrogerai, et réponds-moi.
8 “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
Est-ce que tu rendras vain mon jugement; et me condamneras-tu, pour que toi, tu sois justifié?
9 Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
Et as-tu un bras comme Dieu, et tonnes-tu d’une voix semblable?
10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
Environne-toi de majesté, et élève-toi dans les airs, et sois glorieux, et revêts-toi de splendides vêtements.
11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
Dissipe les superbes dans ta fureur, et d’un regard humilie tout arrogant.
12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
Regarde tous les superbes et confonds-les; et brise les impies en leur lieu.
13 Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
Cache-les dans la poussière tous ensemble, et plonge leurs faces dans la fosse.
14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
Et moi, je confesserai que ta droite peut te sauver.
15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
Vois, Béhémoth que j’ai fait avec toi mangera du foin comme le bœuf.
16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
Sa force est dans ses reins, et sa vertu dans le nombril de son ventre.
17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
Il serre sa queue qui est semblable à un cèdre; les nerfs de ses cuisses sont entrelacés.
18 Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
Ses os sont des tuyaux d’airain, ses cartilages comme des lames de fer.
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
C’est lui qui est le commencement des voies de Dieu; celui qui l’a fait appliquera son glaive.
20 Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
C’est pour lui que les montagnes portent des herbes; toutes les bêtes de la campagne viendront se jouer là.
21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
Il dort sous l’ombre, dans le secret des roseaux et dans des lieux humides.
22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
Des ombres couvrent son ombre, et les saules du torrent l’environneront.
23 Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
Voici qu’il absorbera un fleuve, et il ne s’en étonnera point; il a même la confiance que le Jourdain viendra couler dans sa bouche.
24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?
On le prendra par les yeux comme à l’hameçon, et, avec des harpons, on percera ses narines.

< Ayubu 40 >