< Ayubu 40 >
1 Bwana akamwambia Ayubu:
and to answer LORD [obj] Job and to say
2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
to contend with Almighty faultfinder to rebuke god to answer her
3 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
and to answer Job [obj] LORD and to say
4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
look! to lighten what? to return: reply you hand my to set: put upon lip my
5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
one to speak: speak and not to answer and two and not to add: again
6 Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
and to answer LORD [obj] Job (from *Q(K)*) (tempest *Q(k)*) and to say
7 “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
to gird please like/as great man loin your to ask you and to know me
8 “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
also to break justice: judgement my be wicked me because to justify
9 Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
and if: surely yes arm like/as God to/for you and in/on/with voice like him to thunder
10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
to adorn please pride and height and splendor and glory to clothe
11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
to scatter fury face: anger your and to see: see all proud and to abase him
12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
to see: see all proud be humble him and to tread down wicked underneath: stand them
13 Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
to hide them in/on/with dust unitedness face their to saddle/tie in/on/with to hide
14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
and also I to give thanks you for to save to/for you right your
15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
behold please Behemoth which to make with you grass like/as cattle to eat
16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
behold please strength his in/on/with loin his and strength his in/on/with muscle belly: abdomen his
17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
to sway tail his like cedar sinew (thigh his *Q(K)*) to intertwine
18 Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
bone his channel bronze bone his like/as rod iron
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
he/she/it first: beginning way: conduct God [the] to make him to approach: bring sword his
20 Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
for produce mountain: mount to lift: aid to/for him and all living thing [the] land: wildlife to laugh there
21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
underneath: under lotus to lie down: lay down in/on/with secrecy branch: stem and swamp
22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
to cover him lotus shadow his to turn: surround him willow torrent: river
23 Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
look! to oppress river not to hurry to trust for to burst/come out Jordan to(wards) lip his
24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?
in/on/with eye his to take: take him in/on/with snare to pierce face: nose