< Ayubu 40 >

1 Bwana akamwambia Ayubu:
And YHWH answers Job and says:
2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
“Is the striver with the Mighty instructed? The reprover of God, let him answer it.”
3 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
And Job answers YHWH and says:
4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
“Behold, I have been vile, What do I return to You? I have placed my hand on my mouth.
5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
I have spoken once, and I do not answer, And twice, and I do not add.”
6 Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
And YHWH answers Job out of the whirlwind and says:
7 “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
“Now gird your loins as a man, I ask you, and you cause Me to know.
8 “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
Do you also make My judgment void? Do you condemn Me, That you may be righteous?
9 Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
And do you have an arm like God? And do you thunder with a voice like His?
10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
Now put on excellence and loftiness, Indeed, put on splendor and beauty.
11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
Scatter abroad the wrath of your anger, And see every proud one, and make him low.
12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
See every proud one—humble him, And tread down the wicked in their place.
13 Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
Hide them in the dust together, Bind their faces in secret.
14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
And even I praise you, For your right hand gives salvation to you.
15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
Now behold, behemoth, That I made with you: He eats grass as an ox.
16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
Now behold, his power [is] in his loins, And his strength in the muscles of his belly.
17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
He bends his tail as a cedar, The sinews of his thighs are wrapped together,
18 Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
His bones [are] tubes of bronze, His bones [are] as a bar of iron.
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
He [is] a beginning of the ways of God, His Maker [alone] brings His sword near;
20 Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
For mountains bear food for him, And all the beasts of the field play there.
21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
He lies down under shades, In a secret place of reed and marsh.
22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
Shades cover him, [with] their shadow, Willows of the brook cover him.
23 Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
Behold, a flood oppresses—he does not hurry, He is confident though Jordan Comes forth to his mouth.
24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?
Does [one] take him by his eyes? Does [one] pierce the nose with snares?”

< Ayubu 40 >