< Ayubu 40 >
1 Bwana akamwambia Ayubu:
Moreover the LORD answered Job, and said:
2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
Shall he that reproveth contend with the Almighty? He that argueth with God, let him answer it.
3 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
Then Job answered the LORD, and said:
4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
Behold, I am of small account; what shall I answer Thee? I lay my hand upon my mouth.
5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
Once have I spoken, but I will not answer again; yea, twice, but I will proceed no further.
6 Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
Then the LORD answered Job out of the whirlwind, and said:
7 “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
Gird up thy loins now like a man; I will demand of thee, and declare thou unto Me.
8 “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
Wilt thou even make void My judgment? Wilt thou condemn Me, that thou mayest be justified?
9 Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
Or hast thou an arm like God? And canst thou thunder with a voice like Him?
10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
Deck thyself now with majesty and excellency, and array thyself with glory and beauty.
11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
Cast abroad the rage of thy wrath; and look upon every one that is proud, and abase him.
12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
Look on every one that is proud, and bring him low; and tread down the wicked in their place.
13 Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
Hide them in the dust together; bind their faces in the hidden place.
14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
Then will I also confess unto thee that thine own right hand can save thee.
15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
Behold now behemoth, which I made with thee; he eateth grass as an ox.
16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
Lo now, his strength is in his loins, and his force is in the stays of his body.
17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
He straineth his tail like a cedar; the sinews of his thighs are knit together.
18 Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
His bones are as pipes of brass; his gristles are like bars of iron.
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
He is the beginning of the ways of God; He only that made him can make His sword to approach unto him.
20 Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
Surely the mountains bring him forth food, and all the beasts of the field play there.
21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
He lieth under the lotus-trees, in the covert of the reed, and fens.
22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
The lotus-trees cover him with their shadow; the willows of the brook compass him about.
23 Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
Behold, if a river overflow, he trembleth not; he is confident, though the Jordan rush forth to his mouth.
24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?
Shall any take him by his eyes, or pierce through his nose with a snare?