< Ayubu 40 >

1 Bwana akamwambia Ayubu:
2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
Will he who is protesting give teaching to the Ruler of all? Let him who has arguments to put forward against God give an answer.
3 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
And Job said in answer to the Lord,
4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
Truly, I am of no value; what answer may I give to you? I will put my hand on my mouth.
5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
I have said once, and even twice, what was in my mind, but I will not do so again.
6 Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
Then the Lord made answer to Job out of the storm-wind, and said,
7 “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
Get your strength together like a man of war: I will put questions to you, and you will give me the answers.
8 “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
Will you even make my right of no value? will you say that I am wrong in order to make clear that you are right?
9 Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
Have you an arm like God? have you a voice of thunder like his?
10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
Put on the ornaments of your pride; be clothed with glory and power:
11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
Let your wrath be overflowing; let your eyes see all the sons of pride, and make them low.
12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
Send destruction on all who are lifted up, pulling down the sinners from their places.
13 Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
Let them be covered together in the dust; let their faces be dark in the secret place of the underworld.
14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
Then I will give praise to you, saying that your right hand is able to give you salvation.
15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
See now the Great Beast, whom I made, even as I made you; he takes grass for food, like the ox.
16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
His strength is in his body, and his force in the muscles of his stomach.
17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
His tail is curving like a cedar; the muscles of his legs are joined together.
18 Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
His bones are pipes of brass, his legs are like rods of iron.
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
He is the chief of the ways of God, made by him for his pleasure.
20 Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
He takes the produce of the mountains, where all the beasts of the field are at play.
21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
He takes his rest under the trees of the river, and in the pool, under the shade of the water-plants.
22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
He is covered by the branches of the trees; the grasses of the stream are round him.
23 Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
Truly, if the river is overflowing, it gives him no cause for fear; he has no sense of danger, even if Jordan is rushing against his mouth.
24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?
Will anyone take him when he is on the watch, or put metal teeth through his nose?

< Ayubu 40 >