< Ayubu 40 >

1 Bwana akamwambia Ayubu:
Og HERREN svarede Job og sagde:
2 “Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
Vil den trættekære tvistes med den Almægtige? Han, som revser Gud, han svare herpå!
3 Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
Da svarede Job HERREN og sagde:
4 “Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
Se, jeg er ringe, hvad skal jeg svare? Jeg lægger min Hånd på min Mund!
5 Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
Een Gang har jeg talt, gentager det ikke, to Gange, men gør det ej mer!
6 Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
Da svarede HERREN Job ud fra Stormvejret og sagde:
7 “Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
"Omgjord som en Mand dine Lænder, jeg vil spørge, og du skal lære mig!
8 “Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
Mon du vil gøre min Ret til intet, dømme mig, for af du selv kan få Ret?
9 Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
Har du en Arm som Gud, kan du tordne med Brag som han?
10 Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
Smyk dig med Højhed og Storhed, klæd dig i Glans og Herlighed!
11 Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
Udgyd din Vredes Strømme, slå de stolte ned med et Blik,
12 mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
bøj med et Blik de stolte og knus på Stedet de gudløse,
13 Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
skjul dem i Støvet til Hobe og lænk deres Åsyn i Skjulet!
14 Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
Så vil jeg også love dig for Sejren, din højre har vundet.
15 “Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
Se Nilhesten! Den har jeg skabt såvel som dig. Som Oksen æder den Græs.
16 Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
Se, hvilken Kraft i Lænderne og hvilken Styrke i Bugens Muskler!
17 Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
Halen holder den stiv som en Ceder, Bovens Sener er flettet sammen;
18 Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
dens Knogler er Rør af, Kobber, Benene i den som Stænger af Jern.
19 Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
Den er Guds ypperste Skabning, skabt til at herske over de andre;
20 Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
thi Foder til den bærer Bjergene, hvor Markens Vildt har Legeplads.
21 Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
Den lægger sig hen under Lotusbuske, i Skjul af Siv og Rør;
22 Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
Lotusbuskene giver den Tag og Skygge, Bækkens Pile yder den Hegn.
23 Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
Den taber ej Modet, når Jordan stiger, er rolig, om Strømmen end svulmer mod dens Gab.
24 Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?
Hvem kan gribe den i dens Tænder og trække Reb igennem dens Snude?

< Ayubu 40 >