< Ayubu 39 >
1 “Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa? Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?
¿Sabes tú el tiempo en qué paren las cabras monteses? ¿o miraste tú las ciervas, cuando están pariendo?
2 Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo? Je, unajua majira yao ya kuzaa?
¿Contaste tú los meses de su preñez? ¿y sabes el tiempo cuando han de parir?
3 Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao; utungu wa kuzaa unakoma.
Como se encorvan, quebrantan sus hijos, pasan sus dolores:
4 Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani; huenda zao wala hawarudi tena.
Como después sanan los hijos, crecen con el grano: salen, y nunca más vuelven a ellas.
5 “Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru? Ni nani aliyezifungua kamba zake?
¿Quién echó libre al asno montés? ¿y quién soltó sus ataduras?
6 Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake, nchi ya chumvi kuwa makao yake.
Al cual yo puse casa en la soledad, y sus moradas en la tierra salada.
7 Huzicheka ghasia za mji, wala hasikii kelele za mwendesha gari.
Ríese de la multitud de la ciudad: no oye las voces del pechero.
8 Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho na kutafuta kila kitu kibichi.
Lo oculto de los montes es su pasto, y anda buscando todo lo que está verde.
9 “Je, nyati atakubali kukutumikia? Atakaa karibu na hori lako usiku?
¿Querrá el unicornio servirte a ti, ni quedar a tu pesebre?
10 Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba? Je, atalima mabonde nyuma yako?
¿Atarás tú al unicornio con su coyunda para el surco? ¿labrará los valles en pos de ti?
11 Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi? Utamwachia yeye kazi zako nzito?
¿Confiarás tú en él, por ser grande su fortaleza, y fiarás de él tu labor?
12 Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?
¿Fiarás de él que te tornará tu simiente, y que allegará en tu era?
13 “Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha, lakini hayawezi kulinganishwa na mabawa na manyoya ya korongo.
¿Hiciste tú las alas alegres del avestruz: los cañones y la pluma de la cigüeña?
14 Huyataga mayai yake juu ya ardhi, na kuyaacha yapate joto mchangani,
La cual desampara en la tierra sus huevos, y sobre el polvo los calienta,
15 bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda, kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.
Y olvídase de que los pisará algún pie, y que los quebrará alguna bestia del campo.
16 Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake; hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,
Endurécese para con sus hijos, como si no fuesen suyos, no temiendo de que su trabajo haya sido en vano:
17 kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima, wala hakumpa fungu la akili njema.
Porque Dios la hizo olvidar de sabiduría, y no le dio inteligencia.
18 Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia, humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.
A su tiempo se levanta en alto, y se burla del caballo, y del que sube en él.
19 “Je, wewe humpa farasi nguvu au kuivika shingo yake manyoya marefu?
¿Diste tú al caballo la fortaleza? ¿vestiste tú su cerviz de relincho?
20 Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige, akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?
¿Espantarle has tú como a alguna langosta, en cuya nariz hay fuerza para espantar?
21 Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake, husonga mbele kukabiliana na silaha.
Escarba la tierra, alégrase en su fuerza, sale al encuentro de las armas:
22 Huicheka hofu, haogopi chochote, wala haukimbii upanga.
Hace burla del espanto, y no teme; ni vuelve el rostro delante de la espada.
23 Podo hutoa sauti kando yake, pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.
Contra él suena la aljaba, el hierro de la lanza, y de la pica;
24 Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi, wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.
Y él con ímpetu y furor escarba la tierra, y no estima el sonido de la bocina.
25 Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’ Hunusa harufu ya vita toka mbali, sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.
Entre las bocinas dice: ¡Ea! y desde lejos huele la batalla, el estruendo de los príncipes, y el clamor.
26 “Je, mwewe huruka kwa hekima yako na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?
¿Vuela el gavilán por tu industria, y extiende sus alas hacia el mediodía?
27 Je, tai hupaa juu kwa amri yako na kujenga kiota chake mahali pa juu?
¿Enaltécese el águila por tu mandamiento, y pone en alto su nido:
28 Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku; majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.
Habita, y está en la piedra en la cumbre del peñasco, y de la roca?
29 Kutoka huko hutafuta chakula chake; macho yake hukiona kutoka mbali.
Desde allí asecha la comida: sus ojos consideran muy lejos.
30 Makinda yake hujilisha damu, na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”
Y sus pollos tragan sangre; y adonde hubiere muertos, allí está.