< Ayubu 39 >
1 “Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa? Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?
あなたは岩間のやぎが子を産むときを知っているか。あなたは雌じかが子を産むのを見たことがあるか。
2 Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo? Je, unajua majira yao ya kuzaa?
これらの妊娠の月を数えることができるか。これらが産む時を知っているか。
3 Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao; utungu wa kuzaa unakoma.
これらは身をかがめて子を産み、そのはらみ子を産みいだす。
4 Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani; huenda zao wala hawarudi tena.
その子は強くなって、野に育ち、出て行って、その親のもとに帰らない。
5 “Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru? Ni nani aliyezifungua kamba zake?
だれが野ろばを放って、自由にしたか。だれが野ろばのつなぎを解いたか。
6 Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake, nchi ya chumvi kuwa makao yake.
わたしは荒野をその家として与え、荒れ地をそのすみかとして与えた。
7 Huzicheka ghasia za mji, wala hasikii kelele za mwendesha gari.
これは町の騒ぎをいやしめ、御者の呼ぶ声を聞きいれず、
8 Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho na kutafuta kila kitu kibichi.
山を牧場としてはせまわり、もろもろの青物を尋ね求める。
9 “Je, nyati atakubali kukutumikia? Atakaa karibu na hori lako usiku?
野牛は快くあなたに仕え、あなたの飼葉おけのかたわらにとどまるだろうか。
10 Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba? Je, atalima mabonde nyuma yako?
あなたは野牛に手綱をつけてうねを歩かせることができるか、これはあなたに従って谷を耕すであろうか。
11 Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi? Utamwachia yeye kazi zako nzito?
その力が強いからとて、あなたはこれに頼むであろうか。またあなたの仕事をこれに任せるであろうか。
12 Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?
あなたはこれにたよって、あなたの穀物を打ち場に運び帰らせるであろうか。
13 “Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha, lakini hayawezi kulinganishwa na mabawa na manyoya ya korongo.
だちょうは威勢よくその翼をふるう。しかしこれにはきれいな羽と羽毛があるか。
14 Huyataga mayai yake juu ya ardhi, na kuyaacha yapate joto mchangani,
これはその卵を土の中に捨て置き、これを砂のなかで暖め、
15 bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda, kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.
足でつぶされることも、野の獣に踏まれることも忘れている。
16 Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake; hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,
これはその子に無情であって、あたかも自分の子でないようにし、その苦労のむなしくなるをも恐れない。
17 kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima, wala hakumpa fungu la akili njema.
これは神がこれに知恵を授けず、悟りを与えなかったゆえである。
18 Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia, humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.
これがその身を起して走る時には、馬をも、その乗り手をもあざける。
19 “Je, wewe humpa farasi nguvu au kuivika shingo yake manyoya marefu?
あなたは馬にその力を与えることができるか。力をもってその首を装うことができるか。
20 Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige, akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?
あなたはこれをいなごのように、とばせることができるか。その鼻あらしの威力は恐ろしい。
21 Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake, husonga mbele kukabiliana na silaha.
これは谷であがき、その力に誇り、みずから出ていって武器に向かう。
22 Huicheka hofu, haogopi chochote, wala haukimbii upanga.
これは恐れをあざ笑って、驚くことなく、つるぎをさけて退くことがない。
23 Podo hutoa sauti kando yake, pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.
矢筒はその上に鳴り、やりと投げやりと、あいきらめく。
24 Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi, wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.
これはたけりつ、狂いつ、地をひとのみにし、ラッパの音が鳴り渡っても、立ちどまることがない。
25 Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’ Hunusa harufu ya vita toka mbali, sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.
これはラッパの鳴るごとにハアハアと言い、遠くから戦いをかぎつけ、隊長の大声およびときの声を聞き知る。
26 “Je, mwewe huruka kwa hekima yako na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?
たかが舞いあがり、その翼をのべて南に向かうのは、あなたの知恵によるのか、
27 Je, tai hupaa juu kwa amri yako na kujenga kiota chake mahali pa juu?
わしがかけのぼり、その巣を高い所につくるのは、あなたの命令によるのか。
28 Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku; majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.
これは岩の上にすみかを構え、岩のとがり、または険しい所におり、
29 Kutoka huko hutafuta chakula chake; macho yake hukiona kutoka mbali.
そこから獲物をうかがう。その目の及ぶところは遠い。
30 Makinda yake hujilisha damu, na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”
そのひなもまた血を吸う。おおよそ殺された者のある所には、これもそこにいる」。