< Ayubu 39 >

1 “Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa? Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?
Znaš li kako se legu divokoze? Vidje li kako se mlade košute?
2 Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo? Je, unajua majira yao ya kuzaa?
Izbroji li koliko nose mjeseci, znaš li u koje doba se omlade?
3 Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao; utungu wa kuzaa unakoma.
Sagnuvši se, polegu lanad svoju i breme usred pustinje odlažu,
4 Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani; huenda zao wala hawarudi tena.
a kad im porod ojača, poraste, ostave ga i ne vraćaju mu se.
5 “Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru? Ni nani aliyezifungua kamba zake?
Tko dade divljem magarcu slobodu i tko to oglav skinu njemu s glave?
6 Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake, nchi ya chumvi kuwa makao yake.
U zavičaj mu dadoh ja pustinju i polja slana da ondje živuje.
7 Huzicheka ghasia za mji, wala hasikii kelele za mwendesha gari.
Buci gradova on se podruguje i ne sluša goničevih povika.
8 Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho na kutafuta kila kitu kibichi.
Luta brdima, svojim pašnjacima, u potrazi za zeleni svakakvom.
9 “Je, nyati atakubali kukutumikia? Atakaa karibu na hori lako usiku?
Možeš li slugom učinit' bivola, zadržat' ga noć jednu za jaslama?
10 Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba? Je, atalima mabonde nyuma yako?
Možeš li njega za brazdu prikovat' da ralo vuče po docima tvojim?
11 Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi? Utamwachia yeye kazi zako nzito?
Možeš li se osloniti na njega jer je njegova snaga prevelika i prepustit' mu težak svoj posao?
12 Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?
Misliš li tebi da će se vratiti i na gumno ti dotjerati žito?
13 “Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha, lakini hayawezi kulinganishwa na mabawa na manyoya ya korongo.
Krilima svojim noj trepće radosno, iako krila oskudnih i perja.
14 Huyataga mayai yake juu ya ardhi, na kuyaacha yapate joto mchangani,
On svoja jaja na zemlji ostavlja, povjerava ih pijesku da ih grije,
15 bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda, kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.
ne mareć' što ih zgazit' može noga ili nekakva divlja zvijer zgnječiti.
16 Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake; hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,
S nojićima k'o s tuđima postupa; što mu je trud zaludu, on ne mari.
17 kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima, wala hakumpa fungu la akili njema.
Jer Bog je njega lišio pameti, nije mu dao nikakva razbora.
18 Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia, humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.
Ali kada na let krila raširi, tada se ruga konju i konjaniku.
19 “Je, wewe humpa farasi nguvu au kuivika shingo yake manyoya marefu?
Zar si ti konja obdario snagom zar si mu ti vrat grivom ukrasio?
20 Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige, akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?
Zar ti činiš da skače k'o skakavac, da u strah svakog nagoni hrzanjem?
21 Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake, husonga mbele kukabiliana na silaha.
Kopitom zemlju veselo raskapa, neustrašivo srlja na oružje.
22 Huicheka hofu, haogopi chochote, wala haukimbii upanga.
Strahu se ruga, ničeg se ne boji, ni pred mačem uzmaknuti neće.
23 Podo hutoa sauti kando yake, pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.
Na sapima mu zvekeće tobolac, koplje sijeva i ubojna sulica.
24 Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi, wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.
Bijesan i nestrpljiv guta prostore; kad rog zasvira, tko će ga zadržat':
25 Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’ Hunusa harufu ya vita toka mbali, sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.
na svaki zvuk roga on zarže: Ha! Izdaleka on ljuti boj već njuši, viku bojnu i poklič vojskovođa.
26 “Je, mwewe huruka kwa hekima yako na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?
Zar po promislu tvojem lijeće soko i prema jugu krila svoja širi?
27 Je, tai hupaa juu kwa amri yako na kujenga kiota chake mahali pa juu?
Zar se na nalog tvoj diže orao i vrh timora gnijezdo sebi vije?
28 Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku; majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.
Na litici on stanuje i noćÄi, na grebenima vrleti visokih.
29 Kutoka huko hutafuta chakula chake; macho yake hukiona kutoka mbali.
Odatle na plijen netremice vreba, oči njegove vide nadaleko.
30 Makinda yake hujilisha damu, na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”
Krvlju se hrane njegovi orlići; gdje je ubijenih, tamo je i on.”

< Ayubu 39 >