< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Och Herren svarade Job uti ett väder, och sade:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
Hvilken är den som i sina tankar så fela vill, och talar så med oförnuft?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Gjorda dina länder såsom en man; jag vill fråga dig: Säg, äst du så klok?
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Hvar vast du, då jag grundade jordena? Säg mig:
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
Vetst du, ho henne hafver satt sitt mått; eller ho hafver dragit något snöre öfver henne?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
Eller hvaruppå står hennes fotafäste; eller ho hafver henne en hörnsten lagt;
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
Då morgonstjernorna tillsammans lofvade mig, och all Guds barn fröjdade sig?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
Ho hafver tillslutit hafvet med sina dörrar, då det utbrast såsom utu moderlifve;
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
Då jag klädde det med skyar, och invefvade det i töckno, såsom i lindakläde;
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
Då jag förtog thy dess flod med minom dam, och satte thy bom och dörrar före;
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
Och sade: Allt härintill skall du komma, och icke vidare; här skola dina stolta böljor sätta sig?
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
Hafver du i dinom tid budit morgonen, och vist morgonrodnanom sitt rum;
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
Att jordenes ändar måga fattade varda, och de ogudaktige der utskuddade blifva?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
Inseglet skall sig förvandla såsom ler, så att de skola blifva såsom ett kläde;
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
Och dem ogudaktigom skall deras ljus förtaget varda, och de högfärdigas arm skall sönderbruten varda.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
Hafver du kommit uti hafsens grund, och vandrat uti djupsens fjät?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
Hafva dödsens dörrar någon tid upplåtit sig för dig; eller hafver du sett dörrarna åt mörkret?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
Hafver du förnummit huru bred jorden är? Låt höra, vetst du allt detta?
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
Hvilken är vägen dit, der ljuset bor, och hvilket är mörkrens rum;
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
Att du måtte aftaga dess gränso, och märka stigen till dess hus?
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
Visste du, att du skulle på den tiden född varda, och huru många dina dagar blifva skulle?
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
Hafver du der varit, dädan snön kommer; eller hafver du sett, hvadan haglet kommer;
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
Hvilka jag bevarat hafver intill bedröfvelsens dag, intill stridenes och örligets dag?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
Genom hvilken vägen delar sig ljuset, och östanväder uppkommer på jordena?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
Ho hafver utskift regnskurene sitt lopp, och ljungeldenom och dundrena vägen;
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
Så att det regnar uppå jordena, der ingen är, i öknene, der ingen menniska är;
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
Att det skall uppfylla ödemarken och öknen, och kommer gräset till att växa?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
Ho är regnets fader? Ho hafver födt daggenes droppar?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
Utu hvars lif är isen utgången; och ho hafver födt rimfrostet under himmelen;
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
Att vattnet skulle fördoldt varda såsom under stenar, och djupet blifver ofvanuppå ståndandes?
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
Kan du binda tillsammans sjustjärnornas band, eller upplösa Orions band?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Kan du hemta morgonstjernorna fram i sin tid, eller föra vagnen på himmelen öfver sin barn?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
Vetst du, huru himmelen skall regeras; eller kan du sätta ett herradöme öfver honom på jordene?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
Kan du föra dina dunder högt uppe i skynom, att vattnens myckenhet dig öfvertäcker?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Kan du utsläppa ljungeldar, att de fara åstad, och säga: Här äre vi?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
Ho hafver satt visdomen uti det fördolda? Ho hafver gifvit tankomen förstånd?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
Ho är så vis, att han skyarna räkna kan? Ho kan förstoppa vattuläglarna i himmelen,
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
När stoftet är vått vordet, så att det tillhopalöper, och klimparne låda tillsammans?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
Kan du gifva lejinnone hennes rof i jagtene; och mätta de unga lejonen;
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
Så att de lägga sig uti sitt rum, och stilla ligga i kulone på vakt?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Ho reder korpenom mat, när hans ungar ropa till Gud, och veta icke hvar deras mat är?

< Ayubu 38 >