< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Y RESPONDIÓ Jehová á Job desde un torbellino, y dijo:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
¿Quién es ése que oscurece el consejo con palabras sin sabiduría?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Ahora ciñe como varón tus lomos; yo te preguntaré, y hazme saber tú.
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
¿Dónde estabas cuando yo fundaba la tierra? házme[lo] saber, si tienes inteligencia.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
¿Quién ordenó sus medidas, si lo sabes? ¿ó quién extendió sobre ella cordel?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
¿Sobre qué están fundadas sus basas? ¿ó quién puso su piedra angular,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
Cuando las estrellas todas del alba alababan, y se regocijaban todos los hijos de Dios?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
¿Quién encerró con puertas la mar, cuando se derramaba por fuera [como] saliendo de madre;
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
Cuando puse yo nubes por vestidura suya, y por su faja oscuridad.
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
Y establecí sobre ella mi decreto, y le puse puertas y cerrojo,
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
Y dije: Hasta aquí vendrás, y no pasarás adelante, y ahí parará la hinchazón de tus ondas?
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
¿Has tú mandado á la mañana en tus días? ¿has mostrado al alba su lugar,
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
Para que ocupe los fines de la tierra, y que sean sacudidos de ella los impíos?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
Trasmúdase como lodo bajo de sello, y viene á estar como [con] vestidura:
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
Mas la luz de los impíos es quitada de ellos, y el brazo enaltecido es quebrantado.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
¿Has entrado tú hasta los profundos de la mar, y has andado escudriñando el abismo?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
¿Hante sido descubiertas las puertas de la muerte, y has visto las puertas de la sombra de muerte?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
¿Has tú considerado hasta las anchuras de la tierra? Declara si sabes todo esto.
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
¿Por dónde va el camino á la habitación de la luz, y dónde está el lugar de las tinieblas?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
¿Si llevarás tú [ambas cosas] á sus términos, y entenderás las sendas de su casa?
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
¿Sabíaslo tú porque hubieses ya nacido, ó [porque es] grande el número de tus días?
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
¿Has tú entrado en los tesoros de la nieve, ó has visto los tesoros del granizo,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
Lo cual tengo yo reservado para el tiempo de angustia, para el día de la guerra y de la batalla?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
¿Por qué camino se reparte la luz, y se esparce el viento solano sobre la tierra?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
¿Quién repartió conducto al turbión, y camino á los relámpagos y truenos,
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
Haciendo llover sobre la tierra deshabitada, sobre el desierto, donde no hay hombre,
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
Para hartar la [tierra] desierta é inculta, y para hacer brotar la tierna hierba?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
¿Tiene la lluvia padre? ¿ó quién engendró las gotas del rocío?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
¿De qué vientre salió el hielo? y la escarcha del cielo, ¿quién la engendró?
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
Las aguas se endurecen á manera de piedra, y congélase la haz del abismo.
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
¿Podrás tú impedir las delicias de las Pléyades, ó desatarás las ligaduras del Orión?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
¿Sacarás tú á su tiempo los signos de los cielos, ó guiarás el Arcturo con sus hijos?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
¿Supiste tú las ordenanzas de los cielos? ¿dispondrás tú de su potestad en la tierra?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
¿Alzarás tú á las nubes tu voz, para que te cubra muchedumbre de aguas?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
¿Enviarás tú los relámpagos, para que ellos vayan? ¿y diránte ellos: Henos aquí?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
¿Quién puso la sabiduría en el interior? ¿ó quién dió al entendimiento la inteligencia?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
¿Quién puso por cuenta los cielos con sabiduría? y los odres de los cielos, ¿quién los hace parar,
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
Cuando el polvo se ha convertido en dureza, y los terrones se han pegado unos con otros?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
¿CAZARÁS tú la presa para el león? ¿y saciarás el hambre de los leoncillos,
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
Cuando están echados en las cuevas, ó se están en sus guaridas para acechar?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
¿Quién preparó al cuervo su alimento, cuando sus pollos claman á Dios, bullendo de un lado á otro por carecer de comida?

< Ayubu 38 >