< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Entonces el Señor respondió a Job desde el torbellino:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
“¿Quién es el que cuestiona mi sabiduría hablando con tanta ignorancia?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Prepárate, y sé fuerte, porque voy a interrogarte y debes responderme:
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
“¿Dónde estabas cuando puse los cimientos de la tierra? Dime, si tienes ese conocimiento.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
¿Quién decidió sus dimensiones? ¿No lo sabes? ¿Quién extendió una línea de medición?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
¿Sobre qué se apoyan sus cimientos? ¿Quién puso su piedra angular,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
cuando las estrellas de la mañana cantaron juntas y todos los ángeles gritaban de alegría.
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
“Quien fijó los límites del mar cuando nació?
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
¿Quién la vistió de nubes y la envolvió en un manto de profunda oscuridad?
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
Yo establecí sus límites, marcando sus fronteras.
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
Le dije: ‘Puedes venir aquí, pero no más lejos. Aquí es donde se detienen tus orgullosas olas’.
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
“Durante tu vida, ¿has ordenado alguna vez que comience la mañana?
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
¿Has dicho alguna vez a la aurora dónde debe aparecer para que se apodere de los rincones de la tierra y sacuda a los malvados?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
La tierra se cambia como la arcilla bajo un sello; sus rasgos destacan como una prenda arrugada.
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
La ‘luz’ de los malvados les es quitada; sus actos de violencia son detenidos.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
“¿Has entrado en las fuentes del mar? ¿Has explorado sus profundidades ocultas?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
¿Te han mostrado dónde están las puertas de la muerte? ¿Has visto las puertas de las tinieblas?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
¿Sabes hasta dónde se extiende la tierra? ¡Dime si sabes todo esto!
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
¿En qué dirección vive la luz? ¿Dónde habitan las tinieblas?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
¿Puedes llevarlas a casa? ¿Conoces el camino hacia donde viven?
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
¡Claro que lo sabes, porque ya habías nacido entonces! ¡Has vivido tanto tiempo!
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
“¿Has estado donde se guarda la nieve? ¿Has visto dónde se guarda el granizo?
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
Los he guardado para el tiempo de la angustia, para el día de la guerra y de la batalla.
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
¿Conoces el camino hacia donde viene la luz, o hacia donde sopla el viento del este sobre la tierra?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
¿Quién abre un canal para que fluya la lluvia? ¿Quién crea un camino para el rayo?
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
“¿Quién lleva la lluvia a una tierra deshabitada, a un desierto donde no vive nadie,
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
para regar un páramo reseco y hacer crecer la hierba verde?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
¿Tiene la lluvia un padre? ¿Quién fue el padre de las gotas de rocío?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
¿Quién fue la madre del hielo? ¿Tiene madre la escarcha del aire?
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
El agua se convierte en hielo duro como una roca; su superficie se congela.
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
¿Puedes unir las estrellas de las Pléyades? ¿Puedes soltar el cinturón de la constelación de Orión?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
¿Puedes guiar a las estrellas de Mazarot en el momento adecuado? ¿Puedes dirigir la constelación de la Osa Mayor y sus otras estrellas?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
¿Conoces las leyes de los cielos? ¿Puedes aplicarlas a la tierra?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
“¿Puedes gritarles a las nubes y ordenarles que derramen lluvia sobre ti?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
¿Puedes enviar rayos y dirigirlos, para que te respondan diciendo: ‘Aquí estamos’?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
¿Quién ha puesto la sabiduría dentro de la gente? ¿Quién ha dado entendimiento a la mente?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
¿Quién es tan inteligente como para contar las nubes? ¿Quién puede voltear los cántaros de agua del cielo sobre sus lados
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
cuando el polvo se ha cocido en una masa sólida?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
“¿Puedes cazar una presa para el león? ¿Puedes alimentar a los cachorros de león
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
cuando se agazapan en sus guaridas y acechan en los arbustos?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
¿Quién proporciona alimento al cuervo cuando sus crías claman a Dios, débiles de hambre?”

< Ayubu 38 >