< Ayubu 38 >
1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Tad Tas Kungs Ījabam atbildēja no vētras un sacīja:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
Kas tas tāds, kas (Dieva) padomu aptumšo ar neprātīgiem vārdiem?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Apjoz jel kā vīrs savus gurnus, tad Es tev gribu vaicāt, un tu Mani māci.
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Kur tu biji, kad Es zemei liku pamatu? Izteic to, ja tev ir tāds gudrs prāts.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
Vai tu zini, kas viņai mēru licis, jeb kas pār viņu ir vilcis mēra auklu?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
Uz ko viņas pamati ierakti, jeb kas licis viņas stūra akmeni,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
Kad rīta zvaigznes kopā priecīgi dziedāja, un visi Dieva bērni gavilēja?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
Jeb kas jūru aizslēdzis ar durvīm, kad tā izlauzās, un iznāca kā no mātes miesām,
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
Kad Es to ģērbu ar padebešiem, un krēslībā ietinu tā kā tinamos autos,
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
Kad Es tai noliku Savu robežu, un liku aizšaujamos un durvis,
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
Un sacīju: tiktāl tev būs nākt un ne tālāki, un še būs apgulties taviem lepniem viļņiem?
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
Vai tu savā mūžā rītam licis aust, vai auseklim rādījis savu vietu,
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
Lai satver zemes stūrus, ka tie bezdievīgie no tās top izkratīti;
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
Ka tā pārvēršas kā zieģeļa vasks un visas lietas rādās kā apģērbā,
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
Un bezdievīgiem zūd viņu gaišums, un pacelts elkonis salūst?
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
Vai tu esi nācis līdz jūras avotam un staigājis bezdibeņu dziļumos?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
Vai tev atdarījušies nāves vārti, un vai tu esi redzējis nāves ēnas vārtus?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
Vai esi skatījies līdz pasaules malām? Stāsti, ja tu visu to zini.
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
Kur ir tas ceļš, kur gaisma mājo, un tumsa - kur ir viņas vieta?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
Vai tu to varētu pārvest viņas robežā un izzināt viņas nama ceļus?
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
Tu to zini, jo tai laikā tu biji piedzimis, un tev ir daudz to gadu!
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
Vai tu esi nācis, kur tie sniega krājumi, un vai esi redzējis krusas krājumus,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
Ko Es taupu uz spaidu laiku, uz kaušanas un kara dienu?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
Pa kuru ceļu gaisma dalās un kā austrenis izplešas virs zemes?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
Kas lietum rādījis, kur lai gāžas, un ceļu zibeņiem un pērkoniem,
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
Ka lietus līst, kur cilvēka nav, tuksnesī, kur neviens nedzīvo,
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
Ka viņš dzirdina tukšo posta vietu un zālītei liek dīgt?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
Vai lietum ir tēvs, vai kas dzemdinājis rasas lāsi?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
No kura klēpja cēlies ledus, un no kā dzimusi debess salna,
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
Ka ūdeņi sastingst kā akmens, un jūras dziļumi aizsalst cieti?
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
Vai tu vari sasiet Sietiņa saites, vai atraisīt Orijona zvaigžņu saiti?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Vai tu zvaigznes vari izvest savā laikā un vadīt debess vāģus un viņu ratus?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
Vai tu zini debess likumus, jeb vai proti, kā tie valda virs zemes?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
Vai tu savu balsi vari pacelt uz padebešiem, lai ūdeņi plūst zemē uz tevi?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Vai vari sūtīt zibeņus, ka tie iet un uz tevi saka: redzi, še mēs esam?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
Kas lika gudrību tumšos mākoņos un prātu debess spīdumos?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
Kas skaita mākoņus ar gudrību, un kas māk apgāzt padebešus,
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
Ka pīšļi top aplieti, ka tie saskrien un salīp pītēs?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
Vai tu māki medīt laupījumu priekš lauvas un pildīt jauno lauvu tukšo vēderu,
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
Kad tie nogulstas alās un biezos krūmos glūn?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Kas gādā krauklim barību, kad viņa bērni uz Dievu brēc un šurpu turpu skraida, kad nav ko ēst?