< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
ויען-יהוה את-איוב מנהסערה (מן הסערה) ויאמר
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
מי זה מחשיך עצה במלין-- בלי-דעת
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
אזר-נא כגבר חלציך ואשאלך והודיעני
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
איפה היית ביסדי-ארץ הגד אם-ידעת בינה
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
מי-שם ממדיה כי תדע או מי-נטה עליה קו
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
על-מה אדניה הטבעו או מי-ירה אבן פנתה
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
ברן-יחד כוכבי בקר ויריעו כל-בני אלהים
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
ויסך בדלתים ים בגיחו מרחם יצא
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
בשומי ענן לבשו וערפל חתלתו
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
ואשבר עליו חקי ואשים בריח ודלתים
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
ואמר--עד-פה תבוא ולא תסיף ופא-ישית בגאון גליך
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
המימיך צוית בקר ידעתה שחר (ידעת השחר) מקמו
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
לאחז בכנפות הארץ וינערו רשעים ממנה
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
תתהפך כחמר חותם ויתיצבו כמו לבוש
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
וימנע מרשעים אורם וזרוע רמה תשבר
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
הבאת עד-נבכי-ים ובחקר תהום התהלכת
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
הנגלו לך שערי-מות ושערי צלמות תראה
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
התבננת עד-רחבי-ארץ הגד אם-ידעת כלה
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
אי-זה הדרך ישכן-אור וחשך אי-זה מקמו
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
כי תקחנו אל-גבולו וכי-תבין נתיבות ביתו
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
ידעת כי-אז תולד ומספר ימיך רבים
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
הבאת אל-אצרות שלג ואוצרות ברד תראה
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
אשר-חשכתי לעת-צר ליום קרב ומלחמה
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
אי-זה הדרך יחלק אור יפץ קדים עלי-ארץ
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
מי-פלג לשטף תעלה ודרך לחזיז קלות
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
להמטיר על-ארץ לא-איש-- מדבר לא-אדם בו
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
להשביע שאה ומשאה ולהצמיח מצא דשא
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
היש-למטר אב או מי-הוליד אגלי-טל
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
מבטן מי יצא הקרח וכפר שמים מי ילדו
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
כאבן מים יתחבאו ופני תהום יתלכדו
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
התקשר מעדנות כימה או-משכות כסיל תפתח
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
התציא מזרות בעתו ועיש על-בניה תנחם
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
הידעת חקות שמים אם-תשים משטרו בארץ
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
התרים לעב קולך ושפעת-מים תכסך
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
התשלח ברקים וילכו ויאמרו לך הננו
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
מי-שת בטחות חכמה או מי-נתן לשכוי בינה
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
מי-יספר שחקים בחכמה ונבלי שמים מי ישכיב
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
בצקת עפר למוצק ורגבים ידבקו
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
התצוד ללביא טרף וחית כפירים תמלא
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
כי-ישחו במעונות ישבו בסכה למו-ארב
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
מי יכין לערב צידו כי-ילדו אל-אל ישועו יתעו לבלי-אכל

< Ayubu 38 >