< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Alors l'Eternel répondit à Job du milieu d'un tourbillon, et lui dit:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
Qui est celui-ci qui obscurcit le conseil par des paroles sans science?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Ceins maintenant tes reins comme un vaillant homme, et je t'interrogerai, et tu me feras voir quelle est ta science.
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Où étais-tu quand je fondais la terre? dis-le-moi, si tu as de l'intelligence.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
Qui est-ce qui en a réglé les mesures? le sais-tu? ou qui est-ce qui a appliqué le niveau sur elle?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
Sur quoi sont plantés ses pilotis, ou qui est celui qui a posé la pierre angulaire pour la soutenir.
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
Quand les étoiles du matin se réjouissaient ensemble, et que les fils de Dieu chantaient en triomphe?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
Qui est-ce qui a renfermé la mer dans ses bords, quand elle fut tirée de la matrice, [et] qu'elle en sortit?
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
Quand je mis la nuée pour sa couverture, et l'obscurité pour ses langes?
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
Et que j'établis sur elle mon ordonnance, et lui mis des barrières et des portes?
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
Et lui dis: Tu viendras jusque là, et tu ne passeras point plus avant, et ici s'arrêtera l'élévation de tes ondes.
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
As-tu, depuis que tu es au monde, commandé au point du jour; et as-tu montré à l'aube du jour le lieu où elle doit se lever?
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
Afin qu'elle saisisse les extrémités de la terre, et que les méchants se retirent à l'écart,
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
Et qu'elle prenne une nouvelle forme, comme une argile figurée; et que [toutes choses y] paraissent comme avec de [nouveaux] habits,
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
Et que la clarté soit défendue aux méchants, et que le bras élevé soit rompu?
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
Es-tu venu jusqu'aux gouffres de la mer, et t'es-tu promené au fond des abîmes?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
Les portes de la mort se sont-elles découvertes à toi? as-tu vu les portes de l'ombre de la mort?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
As-tu compris toute l'étendue de la terre? si tu l'as toute connue, montre-le.
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
En quel endroit se tient la lumière, et où est le lieu des ténèbres?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
Que tu ailles prendre l'une et l'autre en son quartier, et que tu saches le chemin de leur maison?
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
Tu le sais; car alors tu naquis, et le nombre de tes jours est grand.
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
Es-tu entré dans les trésors de la neige? As-tu vu les trésors de la grêle,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
Laquelle je retiens pour le temps de l'affliction, et pour le jour du choc et du combat?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
Par quel chemin se partage la lumière, [et par quelle voie] le vent d'Orient se répand-il sur la terre?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
Qui est-ce qui a ouvert les conduits aux inondations, et le chemin à l'éclair des tonnerres,
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
Pour faire pleuvoir sur une terre où il n'y a personne, et sur le désert où il ne demeure aucun homme.
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
Pour arroser abondamment les lieux solitaires et déserts, et pour faire pousser le germe de l'herbe?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
La pluie n'a-t-elle point de père? ou qui est-ce qui produit les gouttes de la rosée?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
Du ventre de qui sort la glace? et qui est-ce qui engendre le frimas du ciel?
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
Les eaux se cachent étant durcies comme une pierre, et le dessus de l'abîme se prend.
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
Pourrais-tu retenir les délices de la Poussinière, ou faire lever les tempêtes [qu'excite] la constellation d'Orion?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Peux-tu faire lever en leur temps les signes du Zodiaque? et conduire la petite Ourse avec les étoiles?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
Connais-tu l'ordre des cieux, et disposeras-tu de leur gouvernement sur la terre?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
Crieras-tu à haute voix à la nuée, afin qu'une abondance d'eaux t'arrose?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Enverras-tu les foudres de sorte qu'elles partent, et te disent: Nous voici?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
Qui est-ce qui a mis la sagesse dans les reins? ou qui a donné au cœur l'intelligence?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
Qui est-ce qui a assez d'intelligence pour compter les nuées, et pour placer les outres des cieux,
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
Quand la poudre est détrempée par les eaux qui l'arrosent, et que les fentes [de la terre] viennent à se rejoindre?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
Chasseras-tu de la proie pour le vieux lion, et rassasieras-tu les lionceaux qui cherchent leur vie,
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
Quand ils se tapissent dans leurs antres, et qu'ils se tiennent dans leurs forts aux aguets?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Qui est-ce qui apprête la nourriture au corbeau, quand ses petits crient au [Dieu] Fort, et qu'ils vont errants, parce qu'ils n'ont point de quoi manger?

< Ayubu 38 >