< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Alors Yahweh répondit à Job du sein de la tempête, et dit:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
Quel est celui qui obscurcit ainsi le plan divin, par des discours sans intelligence?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Ceins tes reins, comme un homme: je vais t'interroger, et tu m'instruiras.
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Où étais-tu quand je posais les fondements de la terre? Dis-le, si tu as l'intelligence.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
Qui en a fixé les dimensions? Le sais-tu? Qui a tendu sur elle cordeau?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
Sur quoi ses bases reposent-elles, ou qui en a posé la pierre angulaire,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
quand les astres du matin chantaient en chœur, et que tous les fils de Dieu poussaient des cris d'allégresse?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
Qui a fermé la mer avec des portes, lorsqu'elle sortit impétueuse du sein maternel;
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
quand je lui donnai les nuages pour vêtements, et pour langes d'épais brouillards;
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
quand je lui imposai ma loi, que je lui mis des portes et des verrous,
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
et que je lui dis: « Tu viendras jusqu'ici, non au delà; ici s'arrêtera l'orgueil de tes flots »?
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
As-tu, depuis que tu existes, commandé au matin? As-tu indiqué sa place à l'aurore,
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
pour qu'elle saisisse les extrémités de la terre et qu'elle en secoue les méchants;
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
pour que la terre prenne forme, comme l'argile sous le cachet, et qu'elle se montre parée comme d'un vêtement;
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
pour que les malfaiteurs soient privés de leur lumière, et que le bras levé pour le crime soit brisé?
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
Es-tu descendu jusqu'aux sources de la mer, t'es-tu promené dans les profondeurs de l'abîme?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
Les portes de la mort se sont-elles ouvertes devant toi, as-tu vu les portes du sombre séjour?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
As-tu embrassé l'étendue de la terre? Parle, si tu sais toutes ces choses.
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
Où est le chemin qui conduit au séjour de la lumière, et où se trouve la demeure des ténèbres?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
Tu pourrais les saisir en leur domaine, tu connais les sentiers de leur séjour!...
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
Tu le sais sans doute, puisque tu étais né avant elles; le nombre de tes jours est si grand!...
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
Es-tu entré dans les trésors de la neige? As-tu vu les réservoirs de la grêle,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
que je tiens prêts pour le temps de la détresse, pour les jours de la guerre et du combat?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
Par quelle voie la lumière se divise-t-elle, et le vent d'orient se répand-il sur la terre?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
Qui a ouvert des canaux aux ondées, et tracé une route aux feux du tonnerre,
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
afin que la pluie tombe sur une terre inhabitée, sur le désert où il n'y a point d'hommes;
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
pour qu'elle arrose la plaine vaste et vide, et y fasse germer l'herbe verte!
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
La pluie a-t-elle un père? Qui engendre les gouttes de la rosée?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
De quel sein sort la glace? Et le givre du ciel, qui l'enfante,
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
pour que les eaux durcissent comme la pierre, et que la surface de l'abîme se solidifie?
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
Est-ce toi qui serres les liens des Pléiades, ou pourrais-tu relâcher les chaînes d'Orion?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Est-ce toi qui fais lever les constellations en leur temps, qui conduis l'Ourse avec ses petits?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
Connais-tu les lois du ciel, règles-tu ses influences sur la terre?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
Elèves-tu ta voix jusque dans les nues, pour que des torrents d'eau tombent sur toi?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Est-ce toi qui lâches les éclairs pour qu'ils partent, et te disent-ils: « Nous voici! »
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
Qui a mis la sagesse dans les nuées, ou qui a donné l'intelligence aux météores?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
Qui peut exactement compter les nuées, incliner les urnes du ciel,
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
pour que la poussière se forme en masse solide et que les glèbes adhèrent ensemble?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
Est-ce toi qui chasses pour la lionne sa proie, qui rassasies la faim des lionceaux,
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
quand ils sont couchés dans leur tanière, qu'ils se tiennent en embuscade dans le taillis?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Qui prépare au corbeau sa pâture, quand ses petits crient vers Dieu, qu'ils errent çà et là, sans nourriture?

< Ayubu 38 >