< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Silloin Herra vastasi Jobille tuulispäästä ja sanoi:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
"Kuka olet sinä, joka taitamattomilla puheilla pimennät minun aivoitukseni?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Vyötä nyt kupeesi kuin mies; minä kysyn sinulta, opeta sinä minua.
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Missä olit silloin, kun minä maan perustin? Ilmoita se, jos ymmärryksesi riittää.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
Kuka on määrännyt sen mitat-tottapa sen tiedät-tahi kuka on vetänyt mittanuoran sen ylitse?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
Mihin upotettiin sen perustukset, tahi kuka laski sen kulmakiven,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
kun aamutähdet kaikki iloitsivat ja kaikki Jumalan pojat riemuitsivat?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
Ja kuka sulki ovilla meren, kun se puhkesi ja kohdusta lähti,
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
kun minä panin sille pilven vaatteeksi ja synkeyden kapaloksi,
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
kun minä rakensin sille rajani, asetin sille teljet ja ovet
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
ja sanoin: 'Tähän asti saat tulla, mutta edemmäksi et; tässä täytyy sinun ylväiden aaltojesi asettua'?
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
Oletko eläissäsi käskenyt päivän koittaa tahi osoittanut aamuruskolle paikkansa,
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
että se tarttuisi maan liepeisiin ja pudistaisi jumalattomat siitä pois?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
Silloin se muuttuu niinkuin savi sinetin alla, ja kaikki tulee kuin vaatetettuna esille;
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
jumalattomilta riistetään heidän valonsa, ja kohonnut käsivarsi murskataan.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
Oletko astunut alas meren lähdesuonille asti ja kulkenut syvyyden kuilut?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
Ovatko kuoleman portit sinulle paljastuneet, oletko nähnyt pimeyden portit?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
Käsitätkö, kuinka avara maa on? Ilmoita se, jos kaiken tämän tiedät.
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
Mikä on tie sinne, kussa asuu valo, ja missä on pimeyden asuinsija,
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
että saattaisit sen alueellensa ja tuntisit polut sen majalle?
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
Kaiketi sen tiedät, sillä synnyithän jo silloin, ja onhan päiviesi luku ylen suuri!
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
Oletko käynyt lumen varastohuoneissa, ja oletko nähnyt rakeiden varastot,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
jotka minä olen säästänyt ahdingon ajaksi, sodan ja taistelun päiväksi?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
Mitä tietä jakaantuu valo ja itätuuli leviää yli maan?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
Kuka on avannut kuurnan sadekuurolle ja ukkospilvelle tien,
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
niin että sataa maahan, joka on asumaton, erämaahan, jossa ei ihmistä ole,
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
niin että autio erämaa saa kylläksensä ja maa kasvaa vihannan ruohon?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
Onko sateella isää, tahi kuka on synnyttänyt kastepisarat?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
Kenen kohdusta on jää tullut, ja kuka on synnyttänyt taivaan härmän?
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
Vesi tiivistyy kuin kiveksi, ja syvyyden pinta sulkeutuu kiinni.
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
Taidatko solmita Otavan siteet tahi irroittaa kahleista Kalevanmiekan?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Voitko tuoda esiin eläinradan tähdet aikanansa ja johdattaa Seulaset lapsinensa?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
Tunnetko taivaan lait, tahi sinäkö säädät, miten se maata vallitsee?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
Taidatko korottaa äänesi pilviin ja saada vesitulvan peittämään itsesi?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Taidatko lähettää salamat menemään, niin että sanovat sinulle: 'Katso, tässä olemme'?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
Kuka on pannut viisautta pilvenlonkiin, tahi kuka antoi pilvenhattaroille ymmärrystä?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
Kuka on niin viisas, että laskee pilvien luvun, kuka kaataa tyhjiksi taivaan leilit,
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
kun multa on kuivunut kovaksi kuin valettu ja maakokkareet toisiinsa takeltuneet?"
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
"Sinäkö ajat saaliin naarasleijonalle ja tyydytät nuorten leijonain nälän,
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
kun ne kyyristyvät luolissansa ja ovat väijyksissä tiheikössä?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Kuka hankkii ravinnon kaarneelle, kun sen poikaset huutavat Jumalan puoleen ja lentelevät sinne tänne ruokaa vailla?

< Ayubu 38 >