< Ayubu 38 >
1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Then Yahweh called to Job out of a fierce storm and said,
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
“Who is this who brings darkness to plans by means of words without knowledge?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Now gird up your loins like a man for I will ask you questions, and you must answer me.
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Where were you when I laid the earth's foundations? Tell me, if you have so much understanding.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
Who determined its dimensions? Tell me, if you know. Who stretched the measuring line over it?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
On what were its foundations laid? Who laid its cornerstone
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
when the morning stars sang together and all the sons of God shouted for joy?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
Who shut up the sea with doors when it burst out, as if it had come out of the womb—
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
when I made clouds its clothing, and thick darkness its swaddling bands?
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
That was when I marked out for the sea my boundary, and when I placed its bars and doors,
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
and when I said to it, 'You may come this far, but no farther; here is where I will put a boundary to the pride of your waves.'
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
Have you given orders to the morning, or caused the dawn to know its place,
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
so that it might take hold of the edges of the earth and shake the wicked out of it?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
The earth is changed in appearance like clay changes under a seal; all things on it stand out clearly like the folds of a piece of clothing.
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
From wicked people their 'light' is taken away; their uplifted arm is broken.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
Have you gone to the sources of the waters of the sea? Have you walked in the lowest parts of the deep?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
Have the gates of death been revealed to you? Have you seen the gates of the shadow of death?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
Have you understood the earth in its expanse? Tell me, if you know it all.
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
Where is the way to the resting place of light— as for darkness, where is its place?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
Can you lead light and darkness to their places of work? Can you find the way back to their houses for them?
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
Undoubtedly you know, for you were born then; the number of your days is so large!
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
Have you entered the storehouses for the snow, or have you seen the storehouses for the hail,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
these things that I have kept for times of trouble, for days of battle and war?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
What is the path to where the lightning bolts are distributed or to where the winds are scattered from the east over the earth?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
Who has created the channels for the floods of rain, or who has made a path for the thunder,
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
to cause it to rain on lands where no person exists, and on the wilderness, in which there is no one,
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
to satisfy the devastated and desolate places, and to make the ground sprout with grass?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
Does the rain have a father, or, who fathers the drops of dew?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
Out of whose womb did the ice come? Who bore the white frost out of the sky?
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
The waters hide themselves and become like stone; the surface of the deep becomes frozen.
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
Can you fasten chains on the Pleiades, or undo the cords of Orion?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Can you lead the constellations to appear at their proper times? Can you guide the Bear with its children?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
Do you know the regulations of the sky? Could you set in place the sky's rule over the earth?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
Can you raise your voice up to the clouds, so that an abundance of rainwater may cover you?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Can you send out bolts of lightning that they may go out, that they say to you, 'Here we are'?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
Who has put wisdom in the clouds or has given understanding to the mists?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
Who can number the clouds by his skill? Who can pour out the water skins of the sky
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
when the dust runs into a hard mass and the clods of earth clump tightly together?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
Can you hunt down a victim for a lioness or satisfy the appetite of her young lion cubs
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
when they are crouching in their dens and sheltering in hiding to lie in wait?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Who provides victims for the ravens when their young ones cry out to God and stagger about for lack of food?