< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Then Yahweh responded to Job, out of a storm, and said: —
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
Who is it that darkeneth counsel, by words, without knowledge?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Gird, I pray thee—like a strong man—thy loins, that I may ask thee, and inform thou me:
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Where wast thou, when I founded the earth? Tell, if thou knowest understanding!
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
Who set the measurements thereof, if thou knowest? Or who stretched out over it a line?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
Whereon were the pedestals thereof sunk? Or who laid the corner stone thereof; —
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
When the morning stars sang together, and all the sons of God shouted for joy?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
Or [who] shut in, with double doors, the sea, when, bursting out of the womb, it came forth;
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
When I put a cloud as the garment thereof, and a thick cloud as the swaddling-band thereof;
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
And brake off for it my boundary, and fixed a bar and double doors;
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
And said—Hitherto, shalt thou come, and no further, —and, here, shalt thou set a limit to the majesty of thy waves?
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
Since thy days [began] hast thou commanded the morning? or caused the dawn to know its place;
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
That it might lay hold of the wings of the earth, and the lawless be shaken out of it?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
It transformeth itself like the clay of a seal, so that things stand forth like one arrayed;
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
That their light may be withdrawn from the lawless, and, the lofty arm, be shivered.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
Hast thou entered as far as the springs of the sea? Or, through the secret recesses of the resounding deep, hast thou wandered?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
Have the gates of death been disclosed to thee? And, the gates of the death-shade, couldst thou descry?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
Hast thou well considered, even the breadths of the earth? Tell—if thou knowest it all!
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
Where then is the way, the light shall abide? And, the darkness, where then is its place?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
That thou mayest conduct it unto the bound thereof, and that thou mayest perceive the paths to its house.
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
Thou knowest, for, then, hadst thou been born! And, in number, thy days are many!
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
Hast thou entered into the treasuries of the snow? And, the treasuries of the hail, couldst thou see?
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
Which I have reserved for a time of distress, for the day of conflict and of war?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
Where then is the way the lightning is parted? The east wind spreadeth itself abroad over the earth.
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
Who hath cloven—for the torrent—a channel? Or a way for the lightning of thunders;
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
To give rain over the no-man’s land, the desert, where no son of earth is;
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
To satisfy the wild and the wilderness, to cause to spring forth the meadow of young grass?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
Hath the rain a father? Or who hath begotten the drops of dew?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
Out of whose womb, came forth the ice? And, the hoar-frost of the heavens, who hath given it birth?
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
Like a stone, are the waters congealed, and, the face of the roaring deep, becometh firm!
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
Canst thou bind the fetters of the Pleiades? Or, the bands of Orion, canst thou unloose?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Canst thou bring forth the signs of the Zodiac each in its season? Or, the Bear and her Young, canst thou lead?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
Knowest thou, the statutes of the heavens? Or didst thou appoint his dominion over the earth?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
Canst thou lift up, to the thick cloud, thy voice, and the overflow of waters cover thee?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Canst thou send forth the lightnings, so that they go, and say to thee, Behold us?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
Who hath put—into cloud-forms—wisdom? Or who hath given—to the meteor—understanding?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
Who can count the thin clouds, in wisdom? And, the bottles of the heavens, who can empty out;
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
When the dust is cast into a clod, and the lumps are bound together?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
Wilt thou hunt—for the Lioness—prey? Or, the craving of the Strong Lion, wilt thou satisfy;
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
When they settle down in dens, abide in covert, for lying in wait?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Who prepareth for the Raven his nourishment, —when his young ones—unto GOD—cry out, [when] they wander for lack of food?

< Ayubu 38 >