< Ayubu 38 >
1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
And after Elius had ceased from speaking, the Lord spoke to Job through the whirlwind and clouds, [saying],
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
Who is this that hides counsel from me, and confines words in [his] heart, and thinks to conceal [them] from me?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Gird your loins like a man; and I will ask you, and do you answer me.
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Where was you when I founded the earth? tell me now, if you have knowledge,
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
who set the measures of it, if you know? or who stretched a line upon it?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
On what are its rings fastened? and who is he that laid the corner-stone upon it?
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
When the stars were made, all my angels praised me with a loud voice.
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
And I shut up the sea with gates, when it rushed out, coming forth out its mother's womb.
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
And I made a cloud its clothing, and swathed it in mist.
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
And I set bounds to it, surrounding it with bars and gates.
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
And I said to it, Hitherto shall you come, but you shall not go beyond, but your waves shall be confined within you.
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
Or did I order the morning light in your time; and [did] the morning star [then first] see his appointed place;
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
to lay hold of the extremities of the earth, to cast out the ungodly out of it?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
Or did you take clay of the ground, and form a living creature, and set it with the power of speech upon the earth?
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
And have you removed light from the ungodly, and crushed the arm of the proud?
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
Or have you gone to the source of the sea, and walked in the tracks of the deep?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
And do the gates of death open to you for fear; and did the porters of hell quake when they saw you? ()
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
And have you been instructed in the breadth of the [whole earth] under heaven? tell me now, what is the extent of it?
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
And in what kind of a land does the light dwell? and of what kind is the place of darkness?
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
If you could bring me to their [utmost] boundaries, and if also you know their paths;
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
I know then that you were born at that time, and the number of your years is great.
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
But have you gone to the treasures of snow? and have you seen the treasures of hail?
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
And is there a store [of them], for you against the time of [your] enemies, for the day of wars and battle?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
And whence proceeds the frost? or [whence] is the south wind dispersed over the [whole world] under heaven?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
And who prepared a course for the violent rain, and a way for the thunders;
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
to rain upon the land where [there is] no man, the wilderness, where there is not a man in it; so as to feed the untrodden and uninhabited [land],
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
and cause it to send forth a crop of green herbs?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
Who is the rain's father? and who has generated the drops of dew?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
And out of whose womb comes the ice? and who has produced the frost in the sky,
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
which descends like flowing water? who has terrified the face of the ungodly?
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
And do you understand the band of Pleias, and have you opened the barrier of Orion?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Or will you reveal Mazuroth in his season, and the evening star with his rays? Will you guide them?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
And know you the changes of heaven, or the events which take place together under heaven?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
And will you call a cloud with your voice, and will it obey you with a violent shower of much rain?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
And will you send lightnings, and they shall go? and shall they say to you, What is [your pleasure]?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
And who has given to women skill in weaving, or knowledge of embroidery?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
And who is he that numbers the clouds in wisdom, and has bowed the heaven [down] to the earth?
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
For it is spread out as dusty earth, and I have cemented it as one hewn stone to another.
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
And will you hunt a prey for the lions? and satisfy the desires of the serpents?
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
For they fear in their lairs, and lying in wait couch in the woods.
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
And who has prepared food for the raven? for its young ones wander and cry to the Lord, in search of food.