< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Then the LORD answered Job out of the whirlwind, and said:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
Who is this that darkeneth counsel by words without knowledge?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Gird up now thy loins like a man; for I will demand of thee, and declare thou unto Me.
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Where wast thou when I laid the foundations of the earth? Declare, if thou hast the understanding.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
Who determined the measures thereof, if thou knowest? Or who stretched the line upon it?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
Whereupon were the foundations thereof fastened? Or who laid the corner-stone thereof,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
When the morning stars sang together, and all the sons of God shouted for joy?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
Or who shut up the sea with doors, when it broke forth, and issued out of the womb;
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
When I made the cloud the garment thereof, and thick darkness a swaddlingband for it,
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
And prescribed for it My decree, and set bars and doors,
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
And said: 'Thus far shalt thou come, but no further; and here shall thy proud waves be stayed'?
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
Hast thou commanded the morning since thy days began, and caused the dayspring to know its place;
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
That it might take hold of the ends of the earth, and the wicked be shaken out of it?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
It is changed as clay under the seal; and they stand as a garment.
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
But from the wicked their light is withholden, and the high arm is broken.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
Hast thou entered into the springs of the sea? Or hast thou walked in the recesses of the deep?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
Have the gates of death been revealed unto thee? Or hast thou seen the gates of the shadow of death?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
Hast thou surveyed unto the breadths of the earth? Declare, if thou knowest it all.
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
Where is the way to the dwelling of light, and as for darkness, where is the place thereof;
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
That thou shouldest take it to the bound thereof, and that thou shouldest know the paths to the house thereof?
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
Thou knowest it, for thou wast then born, and the number of thy days is great!
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
Hast thou entered the treasuries of the snow, or hast thou seen the treasuries of the hail,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
Which I have reserved against the time of trouble, against the day of battle and war?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
By what way is the light parted, or the east wind scattered upon the earth?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
Who hath cleft a channel for the waterflood, or a way for the lightning of the thunder;
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
To cause it to rain on a land where no man is, on the wilderness, wherein there is no man;
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
To satisfy the desolate and waste ground, and to cause the bud of the tender herb to spring forth?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
Hath the rain a father? Or who hath begotten the drops of dew?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
Out of whose womb came the ice? And the hoar-frost of heaven, who hath gendered it?
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
The waters are congealed like stone, and the face of the deep is frozen.
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
Canst thou bind the chains of the Pleiades, or loose the bands of Orion?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Canst thou lead forth the Mazzaroth in their season? Or canst thou guide the Bear with her sons?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
Knowest thou the ordinances of the heavens? Canst thou establish the dominion thereof in the earth?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
Canst thou lift up thy voice to the clouds, that abundance of waters may cover thee?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Canst thou send forth lightnings, that they may go, and say unto thee: 'Here we are'?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
Who hath put wisdom in the inward parts? Or who hath given understanding to the mind?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
Who can number the clouds by wisdom? Or who can pour out the bottles of heaven,
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
When the dust runneth into a mass, and the clods cleave fast together?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
Wilt thou hunt the prey for the lioness? Or satisfy the appetite of the young lions,
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
When they couch in their dens, and abide in the covert to lie in wait?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Who provideth for the raven his prey, when his young ones cry unto God, and wander for lack of food?

< Ayubu 38 >