< Ayubu 38 >
1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
Then the LORD answered Job out of the whirlwind and said:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
“Who is this who obscures My counsel by words without knowledge?
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
Now brace yourself like a man; I will question you, and you shall inform Me.
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
Where were you when I laid the foundations of the earth? Tell Me, if you have understanding.
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
Who fixed its measurements? Surely you know! Or who stretched a measuring line across it?
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
On what were its foundations set, or who laid its cornerstone,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
while the morning stars sang together and all the sons of God shouted for joy?
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
Who enclosed the sea behind doors when it burst forth from the womb,
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
when I made the clouds its garment and thick darkness its blanket,
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
when I fixed its boundaries and set in place its bars and doors,
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
and I declared: ‘You may come this far, but no farther; here your proud waves must stop’?
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
In your days, have you commanded the morning or assigned the dawn its place,
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
that it might spread to the ends of the earth and shake the wicked out of it?
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
The earth takes shape like clay under a seal; its hills stand out like the folds of a garment.
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
Light is withheld from the wicked, and their upraised arm is broken.
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
Have you journeyed to the vents of the sea or walked in the trenches of the deep?
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
Have the gates of death been revealed to you? Have you seen the gates of the shadow of death?
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
Have you surveyed the extent of the earth? Tell Me, if you know all this.
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
Where is the way to the home of light? Do you know where darkness resides,
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
so you can lead it back to its border? Do you know the paths to its home?
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
Surely you know, for you were already born! And the number of your days is great!
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
Have you entered the storehouses of snow or observed the storehouses of hail,
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
which I hold in reserve for times of trouble, for the day of war and battle?
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
In which direction is the lightning dispersed, or the east wind scattered over the earth?
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
Who cuts a channel for the flood or clears a path for the thunderbolt,
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
to bring rain on a barren land, on a desert where no man lives,
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
to satisfy the parched wasteland and make it sprout with tender grass?
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
Does the rain have a father? Who has begotten the drops of dew?
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
From whose womb does the ice emerge? Who gives birth to the frost from heaven,
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
when the waters become hard as stone and the surface of the deep is frozen?
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
Can you bind the chains of the Pleiades or loosen the belt of Orion?
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
Can you bring forth the constellations in their seasons or lead out the Bear and her cubs?
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
Do you know the laws of the heavens? Can you set their dominion over the earth?
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
Can you command the clouds so that a flood of water covers you?
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Can you send the lightning bolts on their way? Do they report to you, ‘Here we are’?
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
Who has put wisdom in the heart or given understanding to the mind?
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
Who has the wisdom to count the clouds? Or who can tilt the water jars of the heavens
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
when the dust hardens into a mass and the clods of earth stick together?
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
Can you hunt the prey for a lioness or satisfy the hunger of young lions
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
when they crouch in their dens and lie in wait in the thicket?
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Who provides food for the raven when its young cry out to God as they wander about for lack of food?