< Ayubu 38 >

1 Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:
上主由旋風中向約伯發言說:
2 “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa?
用無知的話,使我的計劃模糊不明的是誰﹖
3 Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu.
你要像勇士束好你的腰,我要問你,請指教我!
4 “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu.
我奠定大地的基礎時,你在那裏﹖你若聰明,儘管說罷!
5 Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?
你知道是誰制定了地的度量,是誰在地上拉了準繩﹖
6 Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,
地的基礎置在何處,是誰立了地的角石﹖
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?
當時星辰一起歌詠,天主的眾子同聲歡呼!
8 “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo,
海水洶湧如出母胎時,是誰用門將海關閉﹖
9 nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene,
是我用雲彩作海的衣裳,用濃霧作海的襁褓。
10 nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,
是我給海劃定了界限,設立了門和閂,
11 niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?
並下令說:「你到此為止,不得越過;你的狂潮到此為止。」
12 “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,
你有生之日,何嘗給晨光出過命令,又何嘗使曙光知道它之所在﹖
13 yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo?
何嘗使光握緊大地四角,將惡人從那裏抖出去﹖
14 Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi.
曙光改變大地,如在膠泥上蓋印;使萬物出現,如著錦衣;
15 Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.
撤去惡人的光明,折斷高舉的手。
16 “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
你曾否到過海的源流,走過深淵的底處﹖
17 Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
死亡的門給你開啟過嗎﹖你見過死影之門嗎﹖
18 Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
你知道大地的廣闊嗎﹖你若知道,請你說罷!
19 “Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
赴光明之所的路是那一條,黑暗的住處在那裏﹖
20 Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
你知道如何引導黑暗到自己的境地,領黑暗回到自己居所的道路上嗎﹖
21 Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
你總該知道,因為你那時已誕生了,而你的年歲已很高。
22 “Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
你到過雪庫,見過雹倉嗎﹖
23 ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
那是我為降災之時,為戰爭之日所存放的。
24 Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
雲霧由那條路散開,東風由那條路吹往大地﹖
25 Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
誰為暴雨啟開閘門,誰為雷電指示道路,
26 ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
好使雨落在無人之境,降在無人的荒野,
27 ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
為潤澤荒野乾旱之地,好使原野中的綠草生長﹖
28 Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
雨有父親嗎﹖誰生了露珠﹖
29 Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
冰出自誰的胎﹖天上的霜是誰生的﹖
30 wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
水怎樣凝結如石﹖深淵的表面怎樣固結﹖
31 “Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
你豈能栓住昂宿的紐結,解開參星的繩索﹖
32 Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
你豈能使晨星按時升出,引導北斗和它的星群﹖
33 Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
你豈知道天體的定律,立定天律以管治大地﹖
34 “Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
你豈能使你的聲音上達雲霄,使雨水沛然降在你處﹖
35 Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
你能否一發令,閃電就發出,且向你說:「我們在這裏﹖」
36 Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
誰將聰明給與鸛鳥,將智慧賦與雄雞﹖
37 Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
誰能憑智力數清雲彩,能傾倒天上的水囊﹖
38 wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
當土壤堅固,泥塊凝結之時,
39 “Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
你是否能為牝獅獵取食物,滿足幼獅的食慾﹖
40 wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
當獅子伏於洞穴,臥於叢林埋伏的時候,
41 Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
當雛鴉無食,往還飛翔,向天主哀鳴的時候,誰能為烏鴉備食﹖

< Ayubu 38 >