< Ayubu 37 >

1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
A esto también se espanta mi corazón, y salta de su lugar.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
Oíd atentamente su voz terrible, y la palabra que sale de su boca.
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
Debajo de todos los cielos lo enderezará, y su luz se extenderá hasta los fines de la tierra.
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
Tras de él bramará el sonido, tronará su valiente voz, y aunque sea oída su voz, no los detiene.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
Tronará Dios maravillosamente con su voz; él hace grandes cosas, y nosotros no lo entendemos.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
Porque a la nieve dice: Sé en la tierra; lluvia tras lluvia, y lluvia tras lluvia en su fortaleza.
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
Con la vehemencia de la lluvia encierra a todo hombre; para que todos los hombres conozcan su voz.
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
La bestia se entrará en su escondrijo, y habitará en sus moradas.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
Del mediodía viene el torbellino, y de los vientos del norte el frío.
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
Por el soplo de Dios se da el hielo, y las anchas aguas son constreñidas.
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
Además de esto con la claridad fatiga las nubes, y las esparce con su luz.
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
Y ellas se revuelven en derredor por sus designios, para hacer sobre la faz del mundo, en la tierra, lo que él les mandó.
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
Unas veces por azote, otras por causa de su tierra, otras por misericordia las hará aparecer.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
Escucha esto, Job: Repósate, y considera las maravillas de Dios.
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
¿Supiste tú por ventura, cuando Dios las ponía en concierto, y hacía levantar la luz de su nube?
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
¿Has conocido tú por ventura las diferencias de las nubes, las maravillas del Perfecto en sabiduría?
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
¿Y eran calientes tus vestidos cuando él daba el reposo a la tierra del mediodía?
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
¿Extendiste tú por ventura con él los cielos firmes como un espejo firme?
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Muéstranos, qué le hemos de decir; para que no hablemos disparates.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
¿Por ventura cuando yo hablare le será contado? ¿Cuando alguno se anegare le será dicho?
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
También alguna vez no se ve la luz clara en los cielos, y pasa un viento y los limpia.
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
De la parte del norte vendrá la serenidad por el Dios terrible de alabanza.
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
El es Todopoderoso, al cual no alcanzamos; grande en potencia, y en juicio, y en multitud de justicia no aflige.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
Por tanto los hombres lo temerán; todos los sabios de corazón no lo verán.

< Ayubu 37 >