< Ayubu 37 >
1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
“Sí, ante esto mi corazón tiembla, y es desplazado de su lugar.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
Escucha, oh, escucha el ruido de su voz, el sonido que sale de su boca.
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
Lo envía bajo todo el cielo, y sus rayos hasta los confines de la tierra.
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
Tras ella ruge una voz. Truena con la voz de su majestad. No se guarda nada cuando se escucha su voz.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
Dios truena maravillosamente con su voz. Él hace grandes cosas, que no podemos comprender.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
Porque dice a la nieve: “Cae sobre la tierra”. también a la lluvia, y a los chubascos de su poderosa lluvia.
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
Él sella la mano de cada hombre, para que todos los hombres a los que ha hecho lo conozcan.
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
Entonces los animales se ponen a cubierto, y permanecen en sus guaridas.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
De su habitación sale la tormenta, y el frío del norte.
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
Por el soplo de Dios se da el hielo, y la anchura de las aguas está congelada.
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
Sí, carga la espesa nube con humedad. Extiende la nube de su rayo.
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
Se ha dado la vuelta gracias a su guía, para que hagan todo lo que él les mande en la superficie del mundo habitable,
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
ya sea por la corrección, o por su tierra, o por la bondad amorosa, que la hace venir.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
“Escucha esto, Job. Quédate quieto y considera las obras maravillosas de Dios.
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
¿Sabes cómo los controla Dios? y hace brillar el rayo de su nube?
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
¿Conoces el funcionamiento de las nubes, las obras maravillosas de aquel que es perfecto en el conocimiento?
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
Tú, cuya ropa es cálida cuando la tierra está quieta a causa del viento del sur?
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
¿Puedes, con él, extender el cielo, que es fuerte como un espejo de metal fundido?
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Enséñanos lo que le vamos a decir, porque no podemos hacer nuestro caso a causa de la oscuridad.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
¿Se le dirá que voy a hablar? ¿O debería un hombre desear ser tragado?
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
Los hombres no ven la luz que brilla en los cielos, pero el viento pasa y los despeja.
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
Del norte viene el esplendor dorado. Con Dios hay una majestuosidad impresionante.
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
No podemos llegar al Todopoderoso. Está exaltado en el poder. Con justicia y gran rectitud, no oprimirá.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
Por eso los hombres lo veneran. No tiene en cuenta a los sabios de corazón”.