< Ayubu 37 >

1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
Mon cœur en est tout tremblant, et il bondit hors de sa place.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
Écoutez, écoutez le bruit de sa voix, et le grondement qui sort de sa bouche!
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
Il l'envoie sous tous les cieux, et son éclair va jusqu'aux extrémités de la terre.
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
Puis, sa voix rugit; il tonne de sa voix magnifique, et il n'épargne pas ses éclairs, quand retentit sa voix.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
Dieu tonne de sa voix merveilleusement; il fait de grandes choses, que nous ne comprenons pas.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
Il dit à la neige: Tombe sur la terre; il le dit aux ondées, aux fortes ondées.
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
Il ferme la main de tous les hommes, afin que tous les hommes, ses créatures, le connaissent,
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
Et les bêtes se retirent dans leurs tanières, et elles demeurent dans leurs repaires.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
Des profondeurs du Sud vient la tempête, et des vents du Nord vient le froid;
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
Par son souffle, Dieu forme la glace, et l'eau qui s'étendait est resserrée.
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
Il charge d'humidité la nue; il disperse les nuages, pleins de ses éclairs,
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
Et ceux-ci se promènent de tous côtés, selon ses directions, pour faire tout ce qu'il commande, sur la face de la terre habitée;
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
Que ce soit pour châtier, ou pour rendre sa terre fertile, ou pour exercer sa bonté, il leur fait atteindre le but.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
Prête l'oreille à cela, Job: arrête-toi, et considère les merveilles de Dieu.
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
Sais-tu comment Dieu les prépare, comment il fait briller la lumière de sa nue?
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
Sais-tu comment se balancent les nuages, cette merveille de celui dont la science est parfaite?
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
Comment tes vêtements sont chauds quand il endort la terre par le vent du Midi?
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
As-tu étendu avec lui les cieux, fermes comme un miroir de métal?
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Apprends-nous donc ce que nous devons dire de lui: car nous ne saurions préparer des discours du sein de nos ténèbres.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
Voudrais-je qu'on lui rapportât ce que je dis? Jamais homme voulut-il être englouti?
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
Et maintenant on ne peut regarder le soleil brillant dans les cieux, quand un vent a passé et les a purifiés,
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
Quand une lueur d'or vient du septentrion. Il y a en Dieu une majesté redoutable.
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
Le Tout-Puissant! nous ne pouvons l'atteindre; il est sublime en puissance, en droit, en justice; il n'opprime personne.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
C'est pourquoi les hommes le craignent. Mais il ne regarde pas ceux qui sont sages en leur cœur.

< Ayubu 37 >