< Ayubu 37 >
1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
À cause de cela aussi mon cœur tremble, et tressaille comme s’il sortait de sa place.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
Écoutez donc le bruit éclatant de sa voix et le grondement qui sort de sa bouche!
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
Il le dirige sous tous les cieux, et son éclair, jusqu’aux extrémités de la terre:
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
Après lui une voix rugit. Il tonne de sa voix majestueuse, et il ne retient pas ses éclairs quand il fait entendre sa voix.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
Dieu tonne merveilleusement de sa voix, faisant de grandes choses que nous ne comprenons pas.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
Car il dit à la neige: Tombe sur la terre! et aussi aux averses de pluie, et aux averses des pluies de sa force.
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
Il met un sceau sur la main de tout homme, afin que tous les hommes connaissent son œuvre.
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
Les bêtes sauvages rentrent dans leurs gîtes, et demeurent dans leurs repaires.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
Des chambres [du midi] vient le tourbillon, et des vents du nord, le froid.
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
Au souffle de Dieu se forme la glace, et la largeur des eaux se resserre.
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
Il charge d’eau le nuage; sa lumière dissipe les nuées;
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
Et sous sa conduite elles tournoient en tout sens, pour accomplir leur œuvre, tout ce qu’il leur commande sur la face du cercle de la terre,
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
Soit qu’il les fasse venir comme verge, ou pour sa terre, ou en bonté.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
Écoute ceci, Job; tiens-toi là, et discerne les œuvres merveilleuses de Dieu.
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
Sais-tu comment Dieu les a disposées et comment il fait briller l’éclair de sa nuée?
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
Comprends-tu le balancement des nuages, les œuvres merveilleuses de celui qui est parfait en connaissance, –
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
Pourquoi tes vêtements sont chauds quand il donne du repos à la terre par le vent du midi?
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
As-tu étendu avec lui la voûte céleste, aussi ferme qu’un miroir de fonte?
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Fais-nous savoir ce que nous lui dirons! Nous ne savons préparer [des paroles], à cause de [nos] ténèbres.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
Lui racontera-t-on que je parle? Si quelqu’un lui parle, il sera sûrement englouti.
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
Et maintenant on ne voit pas la lumière brillante, elle est [cachée] dans les nues; mais le vent passe et les [chasse, et] produit un ciel clair.
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
L’or vient du nord; – par-devers Dieu est la majesté terrible.
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
Le Tout-puissant, nous ne le trouvons pas; grand en force, en jugement et en beaucoup de justice, il n’opprime pas.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
C’est pourquoi les hommes le craindront; aucun des sages de cœur ne le contemplera.