< Ayubu 37 >

1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
« Oui, à cela mon cœur tremble, et est déplacé de sa place.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
Écoutez, oh, écoutez le bruit de sa voix, le son qui sort de sa bouche.
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
Il l'envoie sous tout le ciel, et sa foudre jusqu'aux extrémités de la terre.
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
Après cela, une voix rugit. Il tonne de la voix de sa majesté. Il ne retient rien quand sa voix est entendue.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
Dieu fait retentir sa voix d'une manière merveilleuse. Il fait de grandes choses, que nous ne pouvons pas comprendre.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
Car il dit à la neige: « Tombe sur la terre ». comme pour l'averse de pluie, et aux averses de sa pluie puissante.
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
Il scelle la main de chaque homme, afin que tous les hommes qu'il a créés la connaissent.
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
Puis les animaux se mettent à l'abri, et restent dans leur tanière.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
De sa chambre sort la tempête, et du froid venant du nord.
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
Par le souffle de Dieu, la glace est donnée, et la largeur des eaux est gelée.
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
Oui, il charge d'humidité l'épais nuage. Il répand à l'étranger le nuage de sa foudre.
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
Elle est retournée par ses conseils, pour qu'ils fassent tout ce qu'il leur ordonne sur la surface du monde habitable,
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
que ce soit pour la correction, ou pour son pays, ou par bonté d'âme, qu'il la fait venir.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
« Écoute ceci, Job. Arrêtez-vous, et considérez les merveilles de Dieu.
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
Savez-vous comment Dieu les contrôle? et fait briller les éclairs de sa nuée?
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
Connaissez-vous le fonctionnement des nuages, les merveilles de celui qui est parfait dans la connaissance?
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
Toi dont les vêtements sont chauds quand la terre est immobile à cause du vent du sud?
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
Pouvez-vous, avec lui, déployer le ciel, qui est aussi solide qu'un miroir en métal moulé?
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Apprends-nous ce que nous allons lui dire, car nous ne pouvons pas défendre notre cause à cause de l'obscurité.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
Lui dira-t-on que je veux parler? Ou un homme devrait-il souhaiter être englouti?
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
Maintenant, les hommes ne voient pas la lumière qui brille dans les cieux, mais le vent passe, et les dégage.
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
Du nord vient la splendeur de l'or. Avec Dieu, la majesté est impressionnante.
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
Nous ne pouvons pas atteindre le Tout-Puissant. Il est exalté par le pouvoir. Dans la justice et la grande droiture, il n'opprimera pas.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
C'est pourquoi les hommes le révèrent. Il ne considère pas ceux qui sont sages de cœur. »

< Ayubu 37 >