< Ayubu 37 >

1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
“Yes, at this my heart trembles, and is moved out of its place.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
Hear, oh, hear the noise of his voice, the sound that goes out of his mouth.
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
He sends it out under the whole sky, and his lightning to the ends of the earth.
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
After it a voice roars. He thunders with the voice of his majesty. He doesn’t hold back anything when his voice is heard.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
God thunders marvelously with his voice. He does great things, which we can’t comprehend.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
For he says to the snow, ‘Fall on the earth,’ likewise to the shower of rain, and to the showers of his mighty rain.
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
He seals up the hand of every man, that all men whom he has made may know it.
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
Then the animals take cover, and remain in their dens.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
Out of its room comes the storm, and cold out of the north.
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
By the breath of God, ice is given, and the width of the waters is frozen.
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
Yes, he loads the thick cloud with moisture. He spreads abroad the cloud of his lightning.
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
It is turned around by his guidance, that they may do whatever he commands them on the surface of the habitable world,
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
whether it is for correction, or for his land, or for loving kindness, that he causes it to come.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
“Listen to this, Job. Stand still, and consider the wondrous works of God.
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
Do you know how God controls them, and causes the lightning of his cloud to shine?
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
Do you know the workings of the clouds, the wondrous works of him who is perfect in knowledge?
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
You whose clothing is warm when the earth is still by reason of the south wind?
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
Can you, with him, spread out the sky, which is strong as a cast metal mirror?
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Teach us what we will tell him, for we can’t make our case by reason of darkness.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
Will it be told him that I would speak? Or should a man wish that he were swallowed up?
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
Now men don’t see the light which is bright in the skies, but the wind passes, and clears them.
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
Out of the north comes golden splendor. With God is awesome majesty.
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
We can’t reach the Almighty. He is exalted in power. In justice and great righteousness, he will not oppress.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
Therefore men revere him. He doesn’t regard any who are wise of heart.”

< Ayubu 37 >