< Ayubu 37 >

1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
Also to this it trembles heart my so it may leap from place its.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
Listen completely to [the] raging of voice his and [the] rumbling [which] from mouth his it comes out.
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
Under all the heavens he lets loose it and light his to [the] corners of the earth.
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
After it - it roars a voice he thunders with [the] voice of majesty his and not he holds back them if it is heard voice his.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
He thunders God with voice his wonders [he is] doing great [things] and not we know.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
For to the snow - he says fall earth and [the] shower of rain and [the] shower of [the] rains of strength his.
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
On [the] hand of every person he puts a seal to know all [the] people of work his.
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
And it went an animal in a lair and in dens its it dwells.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
From the chamber it comes a storm-wind and from [the] scattering winds coldness.
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
From [the] breath of God it gives ice and [the] breadth of [the] waters [is] constraint.
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
Also with moisture he burdens [the] dark cloud[s] he scatters [the] cloud of light his.
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
And it round about - [is] turning every way (by guidance his *Q(K)*) to do they all that he commands them - over [the] surface of [the] world [the] earth towards.
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
Whether for a rod or for earth his or for covenant loyalty he makes find it.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
Give ear to! this O Job stand still and consider diligently - [the] wonders of God.
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
¿ Do you know when appoints God on them and he makes shine forth [the] light of cloud his.
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
¿ Do you know on [the] balancing of [the] cloud[s] [the] wondrous works of [one] complete of knowledge.
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
[you] whom Clothes your [are] hot when is still [the] earth from [the] south.
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
Will you spread out? with him clouds hard like a mirror molten.
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Make known to us what? will we say to him not we will set in order because of darkness.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
¿ Will it be recounted to him that I will speak or? did he say anyone that he will be swallowed up.
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
And now - not people see a light [is] brilliant it in the clouds and [the] wind it has passed by and it has cleansed them.
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
From [the] north gold it comes [is] on God awesome of majesty.
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
[the] Almighty Not we have found him exalted of power and justice and greatness of righteousness not he violates.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
Therefore they fear him people not he sees any [people] wise of heart.

< Ayubu 37 >