< Ayubu 37 >
1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
Yea, at this, my heart quaketh, and starteth up out of its place.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
Hear! oh hear! the raging of his voice, A growling sound also, out of his mouth, goeth forth;
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
Under the whole heavens, he letteth it loose, His lightning also, unto the wings of the earth;
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
After it, roareth a voice, He thundereth with his voice of majesty, Nor will he hold them back, when his voice is heard.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
GOD thundereth with his voice, wonderfully, Doing great things, which we cannot know;
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
For, to the snow, he saith, Fall earthwards, —Also to the downpour of rain, yea the downpour of his mighty rains.
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
On the hand of every man, he setteth a seal, that all men may take note of his doing.
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
So then the wild-beast hath gone into covert, and, in its lairs, doth it remain.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
Out of a chamber cometh a storm-wind, and, out of the north, cold.
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
By the breath of GOD, is given—frost, and, the breadth of waters, is congealed;
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
Also, with moisture, burdeneth he the thick cloud, He disperseth his lightning-cloud;
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
Yea, the same, in circles, turneth itself to and fro, by his steering them to their work, whithersoever he commandeth them, over the face of the world, towards the earth.
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
Whether, as a rod, or for his earth, or in lovingkindness, he causeth it to come.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
Give thou ear unto this, O Job, Stay, and consider well the wonders of GOD: —
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
Canst thou got to know of GOD’S giving charge over them, or of the causing of the lightning of his cloud to shine forth?
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
Canst thou get to know concerning the poisings of the thick cloud, the wonders of one who is perfect in knowledge?
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
That thy garments should be hot when he quieteth the earth from the south?
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
Didst thou spread out, with him, the skies, strong as a molten mirror?
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Let us know what we shall say to him, We cannot set in order, by reason of darkness.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
Shall it be declared to him—that I would speak? Were any man to say aught, he might he destroyed?
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
Yet, now, men see not the light, bright though it is in the skies, when, a wind, hath passed over, and cleansed them.
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
Out of the north, a golden light cometh, Upon GOD, is fearful splendour:
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
The Almighty, whom we have not fully found out, is great in vigour, —Neither, justice nor abounding righteousness, will he weaken.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
Therefore, do men revere him, He will not regard any who are wise in heart.