< Ayubu 37 >

1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
At this my heart trembleth, And leapeth out of its place.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
Hear, O hear, the thunder of his voice, And the noise which goeth forth from his mouth!
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
He directeth it under the whole heaven, And his lightning to the ends of the earth.
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
After it the thunder roareth; He thundereth with his voice of majesty, And restraineth it not, when his voice is heard.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
God thundereth with his voice marvellously; Great things doeth he, which we cannot comprehend.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
For he saith to the snow, “Be thou on the earth!” To the shower also, even the showers of his might.
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
He sealeth up the hand of every man, That all men whom he hath made may acknowledge him.
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
Then the beasts go into dens, And abide in their caverns.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
Out of the south cometh the whirlwind, And cold out of the north.
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
By the breath of God ice is formed, And the broad waters become narrow,
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
Yea, with moisture he burdeneth the clouds; He spreadeth abroad his lightning-clouds.
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
They move about by his direction, To execute all his commands throughout the world;
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
Whether he cause them to come for punishment, Or for the land, or for mercy.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
Give ear to this, O Job! Stand still, and consider the wondrous works of God!
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
Dost thou know when God gave commandment to them, And caused the lightning of his cloud to flash?
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
Dost thou understand the balancing of the clouds, The wondrous works of Him that is perfect in knowledge?
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
How thy garments become warm, When he maketh the earth still by the south wind?
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
Canst thou like him spread out the sky, Which is firm like a molten mirror?
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Teach us what we shall say to him! For we cannot set in order our words by reason of darkness.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
Shall it be told him that I would speak? Shall a man speak, that he may be consumed?
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
For now men do not look upon the light, When it is bright in the skies, When the wind hath passed over them, and made them clear.
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
From the north cometh gold; But with God is terrible majesty!
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
The Almighty, we cannot find him out; Great is he in power and justice, Abundant in righteousness; he doth not oppress.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
Therefore let men fear him! Upon none of the wise in heart will he look.

< Ayubu 37 >