< Ayubu 37 >

1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
“At this my heart also pounds and leaps from its place.
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
Listen closely to the thunder of His voice and the rumbling that comes from His mouth.
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
He unleashes His lightning beneath the whole sky and sends it to the ends of the earth.
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
Then there comes a roaring sound; He thunders with His majestic voice. He does not restrain the lightning when His voice resounds.
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
God thunders wondrously with His voice; He does great things we cannot comprehend.
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
For He says to the snow, ‘Fall on the earth,’ and to the gentle rain, ‘Pour out a mighty downpour.’
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
He seals up the hand of every man, so that all men may know His work.
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
The wild animals enter their lairs; they settle down in their dens.
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
The tempest comes from its chamber, and the cold from the driving north winds.
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
By the breath of God the ice is formed and the watery expanses are frozen.
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
He loads the clouds with moisture; He scatters His lightning through them.
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
They swirl about, whirling at His direction, accomplishing all that He commands over the face of all the earth.
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
Whether for punishment or for His land, He accomplishes this in His loving devotion.
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
Listen to this, O Job; stand still and consider the wonders of God.
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
Do you know how God dispatches the clouds or makes the lightning flash?
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
Do you understand how the clouds float, those wonders of Him who is perfect in knowledge?
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
You whose clothes get hot when the land lies hushed under the south wind,
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
can you, like Him, spread out the skies to reflect the heat like a mirror of bronze?
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
Teach us what we should say to Him; we cannot draw up our case when our faces are in darkness.
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
Should He be told that I want to speak? Would a man ask to be swallowed up?
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
Now no one can gaze at the sun when it is bright in the skies after the wind has swept them clean.
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
Out of the north He comes in golden splendor; awesome majesty surrounds Him.
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
The Almighty is beyond our reach; He is exalted in power! In His justice and great righteousness He does not oppress.
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
Therefore, men fear Him, for He is not partial to the wise in heart.”

< Ayubu 37 >