< Ayubu 37 >
1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
為此我心戰慄,跳離它的原位。
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
你們且細聽天主的怒吼聲,聽那從他口中發出的巨響。
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
他令閃電炫耀天下,使之照射地極;
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
接著是雷聲隆隆,那是天主威嚴之聲;他的巨聲一響,沒有什麼能夠阻止。
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
天主每以巨響施行奇事,做出我們莫測的事。
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
他命令雪說:「落在大地上! 」對暴雨說:「傾盆而降! 」
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
人人都停止活動,為叫人知道,這是他的作為。
8 Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
野獸逃回洞穴,臥於自己的窩中。
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
暴風來自南極密宮,嚴寒出自極北之地。
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
天主噓氣成冰,使大水凝成一片。
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
他使雲霧滿涵濕氣,使閃光穿過烏雲。
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
雷電照他的指示旋轉,全照他的命令實行於地面,
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
或為懲戒大地,或為施行恩惠。
14 “Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
約伯啊! 你且側耳細聽這事,立著沉思天主的奇事!
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
你豈能知道天主怎樣發命,怎樣使雲中電光閃爍﹖
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
雲怎樣浮動,全知者的奇妙化工,你豈能明白﹖
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
當南風吹起,大地鎮靜時,你的衣服豈不是發暖﹖
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
你豈能同他展開蒼天,使它堅固如鑄成的銅鏡﹖
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
我們昏愚,不能講話,請教訓我們怎樣答覆他。
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
我說話時,能給他講述些什麼新事﹖世人說話後,豈算是告訴他一項新聞﹖
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
人現今看不見陽光照耀天空,除非等到風過天晴。
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
金光來自北方,天主的左右有威嚴可怕的異光。
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
全能者是我們不可接近的,他的能力和正義,高超絕倫;他公義正道,決不欺壓。
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”
所以人應敬畏他;但那心中自以為聰慧的,他卻不眷顧。