< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
Y AÑADIÓ Eliú, y dijo:
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
Espérame un poco, y enseñarte he; porque todavía [tengo] razones en orden á Dios.
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
Tomaré mi noticia de lejos, y atribuiré justicia á mi Hacedor.
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
Porque de cierto no son mentira mis palabras; contigo [está] el que es íntegro en [sus] conceptos.
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
He aquí que Dios es grande, mas no desestima á nadie: es poderoso en fuerza de sabiduría.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
No otorgará vida al impío, y á los afligidos dará su derecho.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
No quitará sus ojos del justo; antes bien con los reyes los pondrá en solio para siempre, y serán ensalzados.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
Y si estuvieren prendidos en grillos, y aprisionados en las cuerdas de aflicción,
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
El les dará á conocer la obra de ellos, y que prevalecieron sus rebeliones.
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
Despierta además el oído de ellos para la corrección, y díce[les] que se conviertan de la iniquidad.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
Si oyeren, y [le] sirvieren, acabarán sus días en bien, y sus años en deleites.
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
Mas si no oyeren, serán pasados á cuchillo, y perecerán sin sabiduría.
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
Empero los hipócritas de corazón lo irritarán más, y no clamarán cuando él los atare.
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
Fallecerá el alma de ellos en su mocedad, y su vida entre los sodomitas.
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
Al pobre librará de su pobreza, y en la aflicción despertará su oído.
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
Asimismo te apartaría de la boca de la angustia á lugar espacioso, [libre] de todo apuro; y te asentará mesa llena de grosura.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
Mas tú has llenado el juicio del impío, [en vez] de sustentar el juicio y la justicia.
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
Por lo cual [teme] que [en su] ira no te quite con golpe, el cual no puedas apartar de ti con gran rescate.
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
¿Hará él estima de tus riquezas, ni del oro, ni de todas las fuerzas del poder?
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
No anheles la noche, en que desaparecen los pueblos de su lugar.
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
Guárdate, no tornes á la iniquidad; pues ésta escogiste más bien que la aflicción.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
He aquí que Dios es excelso con su potencia: ¿qué enseñador semejante á él?
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
¿Quién le ha prescrito su camino? ¿y quién [le] dirá: Iniquidad has hecho?
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
Acuérdate de engrandecer su obra, la cual contemplan los hombres.
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
Los hombres todos la ven; mírala el hombre de lejos.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
He aquí, Dios es grande, y nosotros no le conocemos; ni se puede rastrear el número de sus años.
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
El reduce las gotas de las aguas, al derramarse la lluvia según el vapor;
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
Las cuales destilan las nubes, goteando en abundancia sobre los hombres.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
¿Quién podrá tampoco comprender la extensión de las nubes, y el sonido estrepitoso de su pabellón?
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
He aquí que sobre él extiende su luz, y cobija [con ella] las raíces de la mar.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
Bien que por esos medios castiga á los pueblos, á la multitud da comida.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
Con las nubes encubre la luz, y mándale [no brillar], interponiendo [aquéllas].
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
Tocante á ella anunciará [el trueno], su compañero, [que hay] acumulación de ira sobre el que se eleva.

< Ayubu 36 >