< Ayubu 36 >
1 Elihu akaendelea kusema:
Entonces Eliú continuó:
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
Espérame un poco y te diré más, porque aún queda algo por decir en defensa de ʼEloha.
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
Desde lejos traeré mi saber y atribuiré justicia a mi Hacedor,
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
porque en verdad mis palabras no son falsas. Contigo está Uno que es perfecto en conocimiento.
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
Ciertamente ʼEL es poderoso, pero no desprecia a nadie. Es poderoso en la fuerza del entendimiento.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
No otorga vida al perverso, pero hace justicia a los afligidos.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
No aparta sus ojos de los justos. Los hace sentar con reyes en el trono para siempre, y serán exaltados.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
Si están presos con grilletes y atrapados con cuerdas de aflicción,
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
los reprende por su obra y por sus transgresiones, porque se exaltaron a sí mismos.
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
Les abre el oído a la corrección y los exhorta a devolverse de la iniquidad.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
Si escuchan y se someten, acaban sus días en prosperidad, y sus años en deleites.
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
Pero si no escuchan, perecen a filo de espada o por su ignorancia.
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
Los impíos de corazón atesoran ira, no claman cuando Él los ata y
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
mueren en la juventud. Sus vidas terminan entre los sodomitas con rituales paganos.
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
Él libra a los afligidos en su aflicción. Abre sus oídos en la opresión.
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
También te sacará de las garras de la angustia a un lugar espacioso y abierto, para servirte una mesa llena de sustancia.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
Pero si tú estás lleno del juicio que merece el perverso, el juicio y la justicia se apoderan de ti.
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
Por lo cual, teme, no sea que en su ira te quite de un golpe, del cual no te pueda librar ni un gran rescate.
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
¿Será suficiente tu clamor para librarte de la angustia o todas las fuerzas de tu poder?
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
No anheles la noche en la cual los pueblos desaparecerán de su lugar.
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
Cuídate de no volver a la iniquidad, porque escogiste ésta en vez de la aflicción.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Ciertamente ʼEL es exaltado en su poder: ¿Quién es un Maestro como Él?
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
¿Quién le señala el camino? ¿Quién le dirá jamás: Cometiste injusticia?
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
Acuérdate de engrandecer su obra, de la cual los hombres cantan.
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
Todos los hombres la contemplan. Los humanos la miran desde lejos.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
Mira, ʼEL es exaltado, y nosotros no lo conocemos. El número de sus años es inescrutable.
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
Él atrae las gotas de agua, y a la lluvia convierte en vapor
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
que destilan las nubes, y vierten en abundancia sobre los hombres.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
¿Quién entenderá el despliegue de las nubes y el estruendo de la bóveda celeste?
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
Ciertamente, despliega su rayo en ella y cubre las profundidades del mar.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
Con tales cosas gobierna a los pueblos y da alimento en abundancia.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
Cubre con sus manos el rayo y lo lanza certero hacia su blanco.
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
El trueno anuncia su presencia, el ganado también, con respecto a la tormenta que se levanta.