< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
Elihú continuó hablando.
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
“Ténganme un poco más de paciencia y déjenme explicarles. Todavía tengo algo que decir en nombre de Dios.
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
Compartiré mis amplios conocimientos, y demostraré que mi Creador tiene razón.
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
Les aseguro que lo que digo no son mentiras, pues soy un hombre cuyos conocimientos son de primer orden.
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
Dios es poderoso, pero no desprecia a nadie; es poderoso en fuerza y comprensión.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
No mantiene vivo al impío, sino que hace justicia al oprimido.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
Siempre presta atención a los que hacen el bien, y los coloca en tronos con los reyes, honrándolos eternamente.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
Si están encadenados, atados con cuerdas de sufrimiento,
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
entonces les explica lo que han hecho: sus pecados arrogantes.
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
Les hace prestar atención y les ordena que dejen de pecar.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
“Si escuchan y hacen lo que Dios dice, vivirán su vida con felicidad.
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
Pero si no escuchan, tendrán una muerte violenta, ignorantes de Dios.
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
Los que rechazan a Dios se aferran a su amargura. Incluso cuando él los disciplina, no claman a él por ayuda.
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
Mueren en su juventud; su vida termina entre los hombres que se prostituyen en el templo.
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
A través del sufrimiento, Dios salva a los que sufren; consigue su atención a través de sus problemas.
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
“Dios está tratando de rescatarte de las fauces de los problemas a un lugar de libertad y seguridad, llenando tu mesa con los mejores alimentos.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
Pero tú te preocupas por la suerte de los malvados; el juicio y la justicia llenan tu mente.
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
Pero ten cuidado de que tu cólera no te seduzca en la burla; y no dejes que el tamaño del ‘soborno’ te conduzcan al pecado.
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
¿Tu grito de auxilio te sostendrá cuando vengan los problemas?
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
No anheles la noche en la que las personas son arrebatadas repentinamente.
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
¡Cuida que no te vuelvas al mal! Porque es por esto que estás siendo probado a través del sufrimiento.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
“¡Mira qué poder tiene Dios! ¿Qué maestro es como él?
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
¿Quién le ha enseñado lo que debe hacer? ¿Quién puede decirle: ‘Has hecho mal’?
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
Al contrario, alábenle por lo que ha hecho, como dicen los cantos.
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
Todo el mundo ha visto la creación de Dios, aunque sólo desde la distancia.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
“Mira qué grande es Dios, más de lo que podemos entender. Nadie puede contar sus años.
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
Él extrae el agua y la destila en rocío y lluvia.
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
Las nubes derraman lluvia, cayendo abundantemente sobre la humanidad.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
¿Alguien puede entender cómo se extienden las nubes, o cómo ruge el trueno desde donde vive?
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
Mira cómo esparce los rayos a su alrededor, y cubre de oscuridad las profundidades del mar.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
Con estas acciones gobierna a los pueblos, les proporciona abundante alimento.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
Tiene el rayo en sus manos y ordena dónde debe caer.
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
El trueno anuncia su presencia: hasta el ganado sabe cuándo se avecina una tormenta”.

< Ayubu 36 >