< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
Elihú je tudi nadaljeval in rekel:
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
»Dovoli mi malo in pokazal ti bom, da bom še govoril za Boga.
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
Svoje spoznanje bom prinesel od daleč in pravičnost pripisal svojemu Stvarniku.
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
Kajti zares moje besede ne bodo napačne. On, ki je popoln v spoznanju, je s teboj.
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
Glej, Bog je mogočen in ne prezira nikogar. Mogočen je v moči in modrosti.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
Ne varuje življenja zlobnih, temveč daje pravico ubogim.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
Svojih oči ne umakne od pravičnih, temveč so oni s kralji na prestolu. Da, utrjuje jih na veke in so povišani.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
In če bodo zvezani v okove in držani v vrveh stiske,
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
tedaj jim kaže njihovo delo in njihove prestopke, ki so jih presegli.
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
Tudi njihovo uho odpira k disciplini in zapoveduje, da se vrnejo od krivičnosti.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
Če ga ubogajo in mu služijo, bodo svoje dni preživeli v uspevanju in svoja leta v užitkih.
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
Toda če ne ubogajo, se bodo pogubili pod mečem in umrli bodo brez spoznanja.
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
Toda hinavci v srcu kopičijo bes. Ne vpijejo, ko jih zvezuje.
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
Umrejo v mladosti in njihovo življenje je med nečistimi.
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
Revnega osvobaja v njegovi stiski in njihova ušesa odpira v zatiranju.
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
Celo tako bi te odstranil iz tesnega na prostran kraj, kjer ni omejenosti in to, kar naj bi bilo postavljeno na tvojo mizo, bi bilo polno tolšče.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
Toda izpolnil si sodbo zlobnega. Sodba in pravica te bosta zgrabili.
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
Ker je bes, pazi, da te ne bi odvzel s svojim udarcem. Potem te velika odkupnina ne more osvoboditi.
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
Bo cenil tvoja bogastva? Ne niti zlata niti vseh sil moči.
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
Ne želi si noči, ko so ljudje iztrebljeni iz svojega kraja.
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
Pazi, ne oziraj se na krivičnost, kajti to si izbral raje kakor stisko.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Glej, Bog s svojo močjo povišuje. Kdo poučuje kakor on?
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
Kdo se mu je pridružil na njegovi poti? Ali kdo lahko reče: ›Počel si krivičnost?‹
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
Spomni se, da poveličuješ njegovo delo, ki ga ljudje gledajo.
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
Vsak človek ga lahko vidi. Človek ga lahko gleda od daleč.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
Glej, Bog je velik in mi ga ne poznamo niti število njegovih let ne more biti preiskano.
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
Kajti kapljice vode dela majhne. Dež izliva glede na njegovo meglico,
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
katero oblaki kapljajo in obilno rosijo na človeka.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
Mar prav tako lahko kdorkoli razume razširjanje oblakov ali zvok njegovega šotora?
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
Glej, svojo svetlobo razširja nanje in pokriva dna morja.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
Kajti z njimi sodi ljudstvu, hrano daje v obilju.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
Z oblaki pokriva svetlobo in ji zapoveduje, naj ne sveti z oblakom, ki prihaja vmes.
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
Njegov hrup govori o tem, tudi živina glede meglice.

< Ayubu 36 >