< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
Prosseguiu Eliú ainda, dizendo:
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
Espera-me um pouco, e eu te mostrarei que ainda há palavras a favor de Deus.
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
Desde longe trarei meu conhecimento, e a meu Criador atribuirei a justiça.
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
Porque verdadeiramente minhas palavras não serão falsas; contigo está um que tem completo conhecimento.
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
Eis que Deus é grande, porém despreza ninguém; grande ele é em poder de entendimento.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
Ele não permite o perverso viver, e faz justiça aos aflitos.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
Ele não tira seus olhos do justo; ao contrário, ele os faz sentar com os reis no trono, e [assim] são exaltados.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
E se estiverem presos em grilhões, e detidos com cordas de aflição,
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
Então ele lhes faz saber as obras que fizeram, e suas transgressões, das quais se orgulharam.
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
E revela a seus ouvidos, para que sejam disciplinados; e lhes diz, para que se convertam da maldade.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
Se ouvirem, e [o] servirem, acabarão seus dias em prosperidade, e seus anos em prazeres.
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
Porém se não ouvirem, perecerão pela espada, e morrerão sem conhecimento.
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
E os hipócritas de coração acumulam a ira [divina]; e quando ele os amarrar, mesmo assim não clamam.
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
A alma deles morrerá em sua juventude, e sua vida entre os pervertidos.
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
Ele livra o aflito de sua aflição, e na opressão ele revela a seus ouvidos.
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
Assim também ele pode te desviar da boca da angústia [para] um lugar amplo, onde não haveria aperto; para o conforto de tua mesa, cheia dos melhores alimentos.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
Mas tu estás cheio do julgamento do perverso; o julgamento e a justiça te tomam.
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
Por causa da furor, [guarda-te] para que não sejas seduzido pela riqueza, nem que um grande suborno te faça desviar.
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
Pode, por acaso, a tua riqueza te sustentar para que não tenhas aflição, mesmo com todos os esforços de [teu] poder?
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
Não anseies pela noite, em que os povos são tomados de seu lugar.
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
Guarda-te, e não te voltes para a maldade; pois por isto que tens sido testado com miséria.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Eis que Deus é exaltado em seu poder; que instrutor há como ele?
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
Quem lhe indica o seu caminho? Quem poderá lhe dizer: Cometeste maldade?
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
Lembra-te de engrandeceres sua obra, a qual os seres humanos contemplam.
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
Todas as pessoas a veem; o ser humano a enxerga de longe.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
Eis que Deus é grande, e nós não o compreendemos; não se pode descobrir o número de seus anos.
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
Ele traz para cima as gotas das águas, que derramam a chuva de seu vapor;
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
A qual as nuvens destilam, gotejando abundantemente sobre o ser humano.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
Poderá alguém entender a extensão das nuvens, [e] os estrondos de seu pavilhão?
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
Eis que estende sobre ele sua luz, e cobre as profundezas do mar.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
Pois por estas coisas ele julga aos povos, e dá alimento em abundância.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
Ele cobre as mãos com o relâmpago, e dá ordens para que atinja o alvo.
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
O trovão anuncia sua presença; o gado também [prenuncia a tempestade] que se aproxima.

< Ayubu 36 >