< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
エリフは重ねて言った、
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
「しばらく待て、わたしはあなたに示すことがある。なお神のために言うべき事がある。
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
わたしは遠くからわが知識を取り、わが造り主に正義を帰する。
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
まことにわたしの言葉は偽らない。知識の全き者があなたと共にいる。
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
見よ、神は力ある者であるが、何をも卑しめられない、その悟りの力は大きい。
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
彼は悪しき者を生かしておかれない、苦しむ者のためにさばきを行われる。
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
彼は正しい者から目を離さず、位にある王たちと共に、とこしえに、彼らをすわらせて、尊くされる。
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
もし彼らが足かせにつながれ、悩みのなわに捕えられる時は、
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
彼らの行いと、とがと、その高ぶったふるまいを彼らに示し、
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
彼らの耳を開いて、教を聞かせ、悪を離れて帰ることを命じられる。
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
もし彼らが聞いて彼に仕えるならば、彼らはその日を幸福に過ごし、その年を楽しく送るであろう。
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
しかし彼らが聞かないならば、つるぎによって滅び、知識を得ないで死ぬであろう。
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
心に神を信じない者どもは怒りをたくわえ、神に縛られる時も、助けを呼び求めることをしない。
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
彼らは年若くして死に、その命は恥のうちに終る。
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
神は苦しむ者をその苦しみによって救い、彼らの耳を逆境によって開かれる。
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
神はまたあなたを悩みから、束縛のない広い所に誘い出された。そしてあなたの食卓に置かれた物はすべて肥えた物であった。
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
しかしあなたは悪人のうくべきさばきをおのれに満たし、さばきと公義はあなたを捕えている。
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
あなたは怒りに誘われて、あざけりに陥らぬように心せよ。あがないしろの大いなるがために、おのれを誤るな。
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
あなたの叫びはあなたを守って、悩みを免れさせるであろうか、いかに力をつくしても役に立たない。
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
人々がその所から断たれるその夜を慕ってはならない。
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
慎んで悪に傾いてはならない。あなたは悩みよりもむしろこれを選んだからだ。
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
見よ、神はその力をもってあがめられる。だれか彼のように教える者があるか。
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
だれか彼のためにその道を定めた者があるか。だれか『あなたは悪い事をした』と言いうる者があるか。
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
神のみわざをほめたたえる事を忘れてはならない。これは人々の歌いあがめるところである。
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
すべての人はこれを仰ぎ見る。人は遠くからこれを見るにすぎない。
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
見よ、神は大いなる者にいまして、われわれは彼を知らない。その年の数も計り知ることができない。
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
彼は水のしたたりを引きあげ、その霧をしたたらせて雨とされる。
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
空はこれを降らせて、人の上に豊かに注ぐ。
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
だれか雲の広がるわけと、その幕屋のとどろくわけとを悟ることができようか。
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
見よ、彼はその光をおのれのまわりにひろげ、また海の底をおおわれる。
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
彼はこれらをもって民をさばき、食物を豊かに賜い、
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
いなずまをもってもろ手を包み、これに命じて敵を打たせられる。
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
そのとどろきは、悪にむかって怒りに燃える彼を現す。

< Ayubu 36 >