< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
エリフまた言詞を繼て曰く
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
暫らく我に容せ我なんぢに示すこと有ん 尚神のために言ふべき事あればなり
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
われ廣くわが知識を取り我の造化主に正義を歸せんとす
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
わが言語は眞實に虚僞ならず 知識の完全き者なんぢの前にあり
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
視よ神は權能ある者にましませども何をも藐視めたまはず その了知の能力は大なり
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
惡しき者を生し存ず 艱難者のために審判を行ひたまふ
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
義しき者に目を離さず 位にある王等とともに永遠に坐せしめて之を貴くしたまふ
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
もし彼ら鏈索に繋がれ 艱難の繩にかかる時は
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
彼らの所行と愆尤とを示してその驕れるを知せ
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
彼らの耳を開きて敎を容れしめ かつ惡を離れて歸れよと彼らに命じたまふ
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
もし彼ら聽したがひて之に事へなば繁昌てその日を送り 樂しくその年を渉らん
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
若かれら聽したがはずば刀劍にて亡び 知識を得ずして死なん
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
しかれども心の邪曲なる者等は忿怒を蓄はへ 神に縛しめらるるとも祈ることを爲ず
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
かれらは年わかくして死亡せ 男娼とその生命をひとしうせん
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
神は艱難者を艱難によりて救ひ 之が耳を虐遇によりて開きたまふ
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
然ば神また汝を狹きところより出して狹からぬ廣き所に移したまふあらん 而して汝の席に陳ぬる物は凡て肥たる物ならん
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
今は惡人の鞫罰なんぢの身に充り 審判と公義となんぢを執ふ
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
なんぢ忿怒に誘はれて嘲笑に陷いらざるやう愼しめよ 收贖の大なるが爲に自ら誤るなかれ
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
なんぢの號叫なんぢを艱難の中より出さんや 如何に力を盡すとも所益あらじ
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
世の人のその處より絶る其夜を慕ふなかれ
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
愼しみて惡に傾むくなかれ 汝は艱難よりも寧ろ之を取んとせり
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
それ神はその權能をもて大なる事を爲したまふ 誰か能く彼のごとくに敎晦を埀んや
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
たれか彼のためにその道を定めし者あらんや 誰かなんぢは惡き事をなせりと言ふことを得ん
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
なんぢ神の御所爲を讚歎ふることを忘れざれ これ世の人の歌ひ崇むる所なり
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
人みな之を仰ぎ觀る 遠き方より人これを視たてまつるなり
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
神は大なる者にいまして我儕かれを知たてまつらず その御年の數は計り知るべからず
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
かれ水を細にして引あげたまへば霧の中に滴り出て雨となるに
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
雲これを降せて人々の上に沛然に灌ぐなり
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
たれか能く雲の舒展る所以 またその幕屋の響く所以を了知んや
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
視よ彼その光明を自己の周圍に繞らし また海の底をも蔽ひたまひ
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
これらをもて民を鞫き また是等をもて食物を豐饒に賜ひ
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
電光をもてその兩手を包み その電光に命じて敵を撃しめたまふ
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
その鳴聲かれを顯はし 家畜すらも彼の來ますを知らすなり

< Ayubu 36 >