< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
Continuant de nouveau, Eliu dit ceci:
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
Ecoute-moi un peu, et je te convaincrai; car j’ai encore à parler en faveur de Dieu.
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
Je reprendrai mes preuves dès le commencement, et je te montrerai que mon créateur est juste.
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
Vraiment, en effet, mes discours sont exempts de mensonge, et ma parfaite science le sera prouvée.
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
Dieu ne rejette point les puissants, puisqu’il est lui-même puissant.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
Mais il ne sauve point les impies, et il fait justice aux pauvres.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
Il ne détournera pas ses yeux du juste; et il place des rois sur le trône pour toujours, et ces rois sont ainsi élevés.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
Et s’ils sont dans les chaînes, et s’ils se trouvent resserrés par les liens de la pauvreté,
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
Il leur montrera leurs œuvres et leurs crimes, parce qu’ils ont été violents.
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
Il découvrira leur oreille pour les reprendre; et il parlera, afin qu’ils reviennent de l’iniquité.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
S’ils écoutent et obéissent, ils accompliront leurs jours dans le bonheur et leurs années dans la gloire.
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
Mais s’ils n’écoutent point, ils passeront par le glaive, et ils périront dans leur folie.
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
Les dissimulés et les astucieux provoquent la colère de Dieu, et ils ne crieront point, lorsqu’ils seront enchaînés.
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
Leur âme mourra dans la tempête, et leur vie parmi les efféminés.
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
Dieu tirera le pauvre de son angoisse, et il découvrira son oreille dans la tribulation.
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
Il te sauvera donc d’un abîme étroit et qui n’a pas de fondement sous lui, et te mettra très au large; et la table où tu prends du repos sera pleine de viandes grasses.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
Ta cause a été jugée comme celle d’un impie; tu recevras selon la cause et le jugement.
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
Que la colère donc ne te surmonte point en sorte que tu opprimes quelqu’un; et que la multitude des dons ne t’incline point vers l’injustice.
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
Abaisse ta grandeur sans que la tribulation t’ y oblige; abaisse aussi les forts et les puissants.
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
N’allonge point la nuit, afin que les peuples, au lieu d’eux, puissent monter jusqu à toi.
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
Prends garde de ne point te porter à l’iniquité; car tu as commencé à la suivre, après la misère qui t’a atteint.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Vois donc! Dieu est élevé dans sa puissance, et nul ne lui est semblable parmi les législateurs.
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
Qui pourra scruter ses voies? ou qui peut lui dire: Vous avez commis une iniquité?
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
Souviens-toi que tu ignores son œuvre, que les hommes ont chantée.
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
Tous les hommes le voient, chacun le considère de loin.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
Vois donc! Dieu est grand, il surpasse notre science, et le nombre de ses années est incalculable.
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
C’est lui qui enlève les gouttes de la pluie, et répand les ondées comme des torrents
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
Qui fondent des nues, lesquelles voilent toutes les régions d’en haut.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
S’il veut étendre les nuées comme sa tente,
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
Et lancer d’en haut des éclairs par sa lumière, il couvrira les extrémités même de la mer.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
Car c’est par ces moyens qu’il juge les peuples, et qu’il donne la nourriture à un grand nombre de mortels.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
Dans ses mains il cache la lumière, et il lui ordonne de paraître de nouveau.
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
Il annonce à celui qu’il aime, qu’elle est son partage, et qu’il peut monter jusqu’à elle,

< Ayubu 36 >