< Ayubu 36 >

1 Elihu akaendelea kusema:
Et Élihu continua et dit:
2 “Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.
Attends-moi un peu, et je te montrerai que j’ai encore des paroles pour Dieu.
3 Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali, nami nitamhesabia haki Muumba wangu.
J’apporterai de loin ce que je sais, et je donnerai justice à mon créateur.
4 Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo; mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.
Car certainement mes discours ne sont pas des mensonges; celui qui est parfait en connaissances est avec toi.
5 “Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu; ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.
Voici, Dieu est puissant et ne méprise personne; il est puissant en force d’intelligence.
6 Hawaachi waovu waendelee kuishi, bali huwapa walioteswa haki yao.
Il ne fait pas vivre le méchant, mais il fait droit aux malheureux.
7 Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki; huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme na kuwatukuza milele.
Il ne retire pas ses yeux de dessus le juste, et [celui-ci] est avec les rois sur le trône, et il les fait asseoir à toujours, et ils sont élevés.
8 Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo, wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,
Et si, liés dans les chaînes, ils sont pris dans les cordeaux du malheur,
9 huwaonyesha yale waliyoyatenda, kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.
Il leur montre ce qu’ils ont fait, et leurs transgressions, parce qu’elles sont devenues grandes;
10 Huwafanya wao kusikia maonyo, na huwaagiza kutubu uovu wao.
Et il ouvre leurs oreilles à la discipline, et leur dit de revenir de l’iniquité.
11 Kama wakitii na kumtumikia, wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio, na miaka yao katika utoshelevu.
S’ils écoutent et le servent, ils accompliront leurs jours dans la prospérité et leurs années dans les choses agréables [de la vie];
12 Lakini wasiposikiliza, wataangamia kwa upanga, nao watakufa pasipo maarifa.
Mais s’ils n’écoutent pas, ils s’en iront par l’épée, et expireront sans connaissance.
13 “Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki; hata anapowafunga, hawamwombi msaada.
Les hypocrites de cœur amassent la colère; ils ne crient pas quand [Dieu] les lie.
14 Wanakufa wangali vijana, miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.
Ils mourront dans la jeunesse, et leur vie est parmi les hommes voués à l’infamie.
15 Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao, na kuzungumza nao katika dhiki zao.
Il délivre le malheureux dans son malheur, et lui ouvre l’oreille dans l’oppression.
16 “Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki, ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi, hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.
Il t’aurait aussi tiré de la gueule de la détresse [et mis] au large, là où il n’y a point de gêne, et la graisse abonderait dans les mets de ta table.
17 Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu; hukumu na haki vimekukamata.
Mais tu es plein des jugements des méchants; le jugement et la justice [te] saisiront.
18 Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri; usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.
Puisqu’il y a de la colère, prends garde qu’elle ne t’enlève par le châtiment; et une grande rançon ne te le fera pas éviter.
19 Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?
Tiendra-t-il compte de tes richesses? Non; – ni de l’or, ni de toutes les ressources de la puissance.
20 Usiutamani usiku uje, ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.
Ne soupire pas après la nuit qui enlèvera les peuples de leur place.
21 Jihadhari usigeukie uovu, ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.
Prends garde à toi! Ne te tourne pas vers l’iniquité, car c’est ce que tu as choisi plutôt que l’affliction.
22 “Mungu ametukuzwa katika nguvu zake. Ni nani aliye mwalimu kama yeye?
Voici, Dieu se montre élevé dans sa puissance: qui enseigne comme lui?
23 Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake, au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?
Qui lui a prescrit son chemin, et qui a dit: Tu as mal agi?
24 Kumbuka kuzitukuza kazi zake, ambazo watu wamezisifu katika wimbo.
Souviens-toi de glorifier son œuvre, que les hommes célèbrent:
25 Wanadamu wote wameiona; watu wanaikazia macho kwa mbali.
Tout homme la contemple, le mortel la regarde de loin.
26 Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu, kupita ufahamu wetu! Hesabu ya miaka yake haitafutiki.
Voici, Dieu est grand, et nous ne le connaissons pas; le nombre de ses années, nul ne le sonde.
27 “Yeye huvuta juu matone ya maji, ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;
Car il attire les gouttes d’eau: des vapeurs qu’il forme elles distillent la pluie,
28 mawingu huangusha chini maji yake, nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.
Que les nuages font couler; ils tombent en gouttes sur les hommes, abondamment.
29 Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu, jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.
Mais qui peut comprendre le déploiement de la nuée, le fracas de son tabernacle?
30 Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka, naye huvifunika vilindi vya bahari.
Voici, il étend sa lumière autour de lui, et couvre le fond de la mer.
31 Hivi ndivyo atawalavyo mataifa, na kuwapa chakula kwa wingi.
Car par ces choses il juge les peuples, il donne la nourriture en abondance.
32 Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi, na kuuagiza kulenga shabaha yake.
Il couvre ses mains de l’éclair, et lui commande où il doit frapper;
33 Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja; hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.
Son bruit l’annonce, le bétail même en présage la venue!

< Ayubu 36 >